Yobu 7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Mwanadamu ana magumu katika dunia, na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara! 2 Yeye ni kama mutumwa anayetamani kivuli, kama mutumishi anayengoja kwa hamu mushahara wake. 3 Basi nimepangiwa miezi na miezi ya taabu, urizi wangu ni kuteseka usiku kwa usiku. 4 Ninapolala ninasema: “Nitaamuka wakati gani?” Maana saa za usiku ni ndefu sana; ninagaagaa katika kitanda mpaka mapambazuko! 5 Mwili wangu umejaa vidudu na uchafu; ngozi yangu imekauka na kutokwa na usaha wa jipu. 6 Siku zangu zinapita mbio kuliko gurudumu la mushonaji, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini. 7 Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona jambo zuri lolote tena. 8 Anayeniona sasa, hataniona tena, mara tu ukiniangalia nitakuwa nimetoweka. 9 Kama vile wingu linavyofifia na kutoweka, ndivyo nao watu wanavyoshukia kuzimu bila kurudi. 10 Anayeondoka harudi tena kwa jamaa yake, na pale alipokuwa anaishi, wanamusahau mara moja. 11 Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu kusema. Nitasema kwa kusongwa kwa roho yangu, nitalalamika kwa uchungu wa nafsi yangu. 12 Mimi ni bahari au nyama mukubwa wa bahari hata upate kuniwekea mulinzi? 13 Nikisema “Kitanda kitanipumzisha, matandiko yangu yatanipunguzia malalamiko yangu”, 14 wewe unakuja kunitia hofu kwa ndoto, unanitisha kwa kuniletea maono, 15 hata ninaona afazali kutundikwa, ninaona heri kufa kuliko kupata mateso haya. 16 Ninayachukia maisha yangu. Sitaishi milele. Muniache, maana siku zangu ni pumzi tu! 17 Mwanadamu ni nini hata umujali? Kwa nini unajishugulisha naye 18 na kuja kumuchunguza kila asubui, na kumupima kila wakati? 19 Utaendelea kuniangalia mpaka wakati gani, bila kuniacha hata nimeze mate? 20 Kama nikitenda zambi, inakuuzi nini, ewe muchungaji wa wanadamu? Mbona umeniweka kuwa shabaha ya mapigo yako? Kwa nini nimekuwa muzigo kwako? 21 Mbona haunisamehe kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi kisha muda kidogo nitalazwa chini katika mavumbi. Utanitafuta, lakini sitakuwa tena! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo