Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yobu akamujibu Elifasi:

2 Heri uchungu wangu ungepimwa, nayo mateso yangu yote yangewekwa katika mizani!

3 Yangekuwa mazito kuliko muchanga wa bahari. Ni kwa hiyo maneno yangu hayana maana!

4 Mishale ya Mungu Mwenye Uwezo imenichoma; nafsi yangu imekunywa sumu yake. Vitisho vya Mungu vimenipata.

5 Punda wa pori analia akiwa na majani, au ngombe akiwa na malisho?

6 Kitu kisichokuwa na onjo kinaweza kuliwa bila chumvi? Sehemu nyeupe ya yai ina utamu wowote?

7 Sina hamu ya kuvigusa vyakula hivyo, hivyo ni vyakula vinavyonichukiza.

8 Heri ningejibiwa kwa ombi langu, Mungu angenipatia kile ninachotamani,

9 angependezwa kunipondaponda, angenyoosha mukono wake juu yangu na kuniua!

10 Hiyo ingekuwa faraja yangu, ningefurahi katika maumivu yasiyokuwa na huruma, kwa sababu sikukataa maagizo ya Mungu Mutakatifu.

11 Sina nguvu ya kuweza kuendelea. Sijui mwisho wangu utakuwa namna gani, nipate kuvumilia.

12 Nguvu zangu ni kama za mawe? Au mwili wangu kama shaba?

13 Kweli kwangu hakuna kitu cha kunisaidia; musaada wowote ni mbali nami.

14 Anayekataa kutendea mema rafiki yake, anakataa kumwogopa Mungu Mwenye Uwezo.

15 Warafiki zangu wamenidanganya kama kijito, wamenidanganya kama mifereji isiyokuwa na maji,

16 ambayo imejaa barafu, na teluji imejificha ndani yake.

17 Wakati wa kipwa inatoweka, wakati wa jua kali inakauka.

18 Wasafiri wanapotea njia zao wakitafuta maji, wanapanda katika jangwa na kukufia kule.

19 Wasafiri toka Tema wanatafutatafuta, wasafiri toka Sheba wanatumainia.

20 Wanachukizwa kwa kutumainia bure, wanafika kwenye vijito hivyo na kuuzika.

21 Ninyi mumekuwa kama vijito hivyo, munaona hasara yangu na kuogopa.

22 Nimesema munipe zawadi? Au munitolee sehemu ya mali zenu?

23 Au muniokoe toka katika mikono ya adui? Au munikomboe toka katika mukono wa watesaji?

24 Munifundishe, nami nitanyamaza. Munieleweshe jinsi nilivyokosa.

25 Maneno ya kweli yana nguvu kubwa! Lakini makaripio yenu yanafaa kwa nini?

26 Munazani kwamba munaweza kuchunguza maneno? Maneno ya mutu aliyekata tamaa ni upepo tu.

27 Ninyi munasubutu hata kuwapigia wayatima kura; munauzisha hata rafiki yenu!

28 Lakini sasa muniangalie tafazali. Mimi sitasema uongo mbele yenu.

29 Tafazali mugeuke, kusikuwe uovu; muache sasa, kwa ajili ya haki yangu.

30 Munazani kwamba nimesema uovu? Munafikiri kwamba mimi siyatambui machungu?

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan