Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yeyote anayeona yule nyama mukubwa anakufa moyo na kuzimia.

2 Hakuna mutu yeyote mukali anayesubutu kumushitua. Nani, basi anayeweza kusimama mbele yangu?

3 Nani aliyenipa kitu, kusudi nipate kumurudishia? Chochote kinachokuwa chini ya mbingu ni changu.

4 Sitaacha kukuelezea juu ya viungo vya yule nyama mukubwa au juu ya nguvu zake na umbo lake zuri.

5 Nani anayeweza kuondoa nguo yake ya inje? Nani anayeweza kutoboa nguo ya chuma anayovaa?

6 Nani anayeweza kufungua kinywa chake? Meno yake pande zote ni kitisho!

7 Mugongo wake umefanywa kwa mistari ya ngao iliyoshikamana pamoja kama kwa muhuri.

8 Kila mumoja umeshikamana na mwingine, hata hewa haiwezi kupenya katikati yake.

9 Imeunganishwa pamoja, hata haiwezekani kuitenganisha.

10 Akipiga chafya, mwangaza unatokea, macho yake yanametameta kama jua inapotokea.

11 Katika kinywa chake kunatokea mienge inayowaka, cheche za moto zinaruka inje.

12 Katika pua yake kunafuka moshi, kama vile chungu kinachochemuka, kama vile nyasi inayowaka.

13 Pumzi yake inawakisha makaa; ulimi wa moto unatoka ndani ya kinywa chake.

14 Shingo yake ina nguvu ajabu, nyama yule anapotokea watu wanapatwa na hofu.

15 Mishipa yake imeshikamana pamoja, imara kama chuma wala haitikisiki.

16 Moyo wake ni mugumu kama jiwe, mugumu kama jiwe la kusagia.

17 Anapoinuka, mashujaa wanashikwa na woga, kwa pigo moja wanazimia.

18 Hakuna upanga unaoweza kumuumiza, wala mukuki, mushale au nguo ya chuma.

19 Kwake chuma ni laini kama unyasi, na shaba kama muti uliooza.

20 Mushale hauwezi kumukimbiza; akitupiwa mawe ya mujeledi anayaona kama maganda.

21 Kwake, gongo ni kama kipande cha bua; anacheka akitupiwa mikuki kwa wingi.

22 Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali; anakwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kulima.

23 Anatikisatikisa bahari kama maji yanayochemuka, anaifanya itoe pofu kama chupa ya mafuta.

24 Anapopita anaacha nyuma kitambulisho kinachoangaa; pofu nyeupe inaonekana ikielea juu ya bahari.

25 Katika dunia hakuna kinachofanana nayo; hicho ni kiumbe kisichokuwa na hofu.

26 Kinawaona kuwa si kitu wote wenye kiburi; hicho ni mufalme wa nyama wote wakali.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan