Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akaendelea kumwambia Yobu:

2 Wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Uwezo? Wewe unayebishana nami Mungu, basi ujibu mambo hayo!

3 Kisha Yobu akamujibu Yawe:

4 Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini? Ninafunga kinywa changu.

5 Nilisubutu kusema na sitasema tena. Nilisema mengi lakini sitaendelea kusema zaidi.

6 Halafu Yawe akamujibu kutoka katika zoruba:

7 Ujikaze kama mwanaume. Nitakuuliza, nawe utanijibu.

8 Unataka kweli kugeuza hukumu yangu, kuniona nina kosa kusudi wewe usikuwe na kosa?

9 Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?

10 Basi, ujionyeshe kuwa na utukufu na ukubwa, ujipambe kwa heshima na mamlaka.

11 Uwamwangie watu hasira yako kubwa; umwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.

12 Umwangalie kila mwenye kiburi na kumuporomosha, uwakanyage waovu pahali wanapokuwa.

13 Uwazike wote pamoja ndani ya udongo; umufunge kila mumoja kwa kifungo cha kifo.

14 Halafu nitakutambua kwa vile nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.

15 Uangalie yule nyama mukubwa kiboko. Nilimwumba kama nilivyokuumba wewe. Yeye anakula majani kama ngombe,

16 lakini ana nguvu ajabu katika mwili wake, na mishipa ya tumbo lake ni imara.

17 Mukia wake ni wenye nguvu kama mwerezi, mishipa ya mapaja yake imeshonwa pamoja.

18 Mifupa yake ni kama mirija ya shaba, mbavu zake ni kama vipande vya chuma.

19 Yeye ni wa kwanza wa ajabu kati ya viumbe vyangu! Ni mimi Muumba wake ninayeweza kumutawala.

20 Milima ambamo nyama wote wa pori wanamochezea inatoa chakula chake.

21 Anajilaza chini ya vichaka vya miiba, na kujificha kati ya matete ndani ya tingitingi.

22 Vivuli vya vichaka vya miiba vinamufunika na vya miti inayoota pembeni ya vijito.

23 Muto ukifurika haogopi, hatishiki hata muto Yordani ukifurikia katika kinywa.

24 Nani anayeweza kuziba macho yake na kumuteka? Nani anayeweza kumutoboa pua kwa mutego?

25 Unaweza kuvua yule nyama mukubwa Leviatani kwa ndoana, au kuufunga ulimi wake kwa kamba?

26 Unaweza kumutia kamba katika pua lake, au kumutoboa taya kwa kulabu?

27 Unazani atakusihi umwachilie? Atazungumuza nawe kwa upole?

28 Atafanya mapatano nawe, umuchukue kuwa mutumishi wako milele?

29 Utacheza naye kama ndege, au kumufunga kamba acheze na wajakazi wako?

30 Unazani wavuvi watashindania bei yake? Wachuuzi watasubutu kumukata na kugawanyana?

31 Wanaweza kuitoboa ngozi yake kwa mikuki, au kichwa chake kwa chuma cha kuvua samaki?

32 Jaribu tu kumugusa: ukifikiri juu ya vita naye, hautarudilia tena kufanya hivyo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan