Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sehemu ya kwanza ya Mazungumuzo ( 4.1–14.22 ) Masemi ya Elifasi

1 Kisha Elifasi wa inchi ya Temani akamujibu Yobu:

2 Mutu akijaribu kukuambia neno utakasirika? Lakini nani anayeweza kujizuia kusema?

3 Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi, na kuiimarisha mikono ya wazaifu.

4 Maneno yako yamewainua moyo, umewaimarisha waliokosa nguvu.

5 Lakini sasa shida imekupata nawe unaregea. Imekugusa, nawe unafazaika.

6 Kumwogopa Mungu si ndilo tegemeo lako? Na ukamilifu wa mwenendo wako si ndilo tumaini lako?

7 Fikiri sasa: nani asiyekuwa na kosa ambaye amepata kuangamia? Au, watu wa usawa wamepata kutupiliwa?

8 Mimi nimeona kwamba wanaopanda uovu na ubaya wanavuna yaleyale.

9 Mungu anawaangamiza kwa pumzi yake; wanateketezwa kwa kuvuma kwa hasira yake.

10 Waovu wananguruma kama simba mukali, lakini meno yao inavunjwa.

11 Simba mwenye nguvu anakufa kwa kukosa chakula, na watoto wa simba dike wanatawanywa!

12 Siku moja, niliambiwa neno kwa siri, sikio langu lilisikia manongonezo yake.

13 Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto, wakati usingizi muzito unawashika watu.

14 Nikashikwa na hofu na kutetemeka; mifupa yangu yote ikagonganagongana.

15 Upepo ukapita mbele ya uso wangu, nywele za mwili wangu zikasimama.

16 Kitu kimoja kikasimama mbele yangu. Nilipokiangalia sikukitambua kabisa. Kulikuwa umbo moja mbele yangu. Kulikuwa kimya, kisha nikasikia sauti:

17 “Mwanadamu anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mutu anaweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

18 Mungu hawaaminie hata watumishi wake, na wamalaika wake anawaona wana kosa.

19 Zaidi sana wanadamu, viumbe vya udongo, watu ambao musingi wao ni mavumbi, ambao wanaweza kupondwapondwa kama chawa!

20 Wanadamu wanaangamia kwa saa chache tu; wanaangamia milele bila kuacha hata alama.

21 Kama uzi unaoshikilia uzima wao ukikatwa, wao wanakufa, tena bila kuwa na hekima”.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan