Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Elihu akaendelea kusema:

2 Musikilize maneno yangu, enyi wenye hekima, munitegee masikio yenu, ninyi wenye ujuzi.

3 Sikio linapima maneno, kama vile ulimi unavyoonja chakula.

4 Basi, tuchague sasa yanayokuwa sawa, tuamue kati yetu yanayokuwa mazuri.

5 Basi, Yobu amesema: “Mimi Yobu sina kosa, Mungu ameniondolea haki yangu.

6 Ingawa sina kosa, ninaonekana kuwa mwongo. Kidonda changu hakiponi ingawa sina kosa.”

7 Ni nani anayekuwa kama Yobu ambaye kwake mazarau ni kama kunywa maji?

8 Anaandamana na watenda maovu, anatembea na watu waovu.

9 Maana amesema: “Mutu hapati faida yoyote na kujisumbua kumupendeza Mungu.”

10 Kwa hiyo munisikilize, enyi wenye ujuzi. Mungu hawezi kufanya uovu hata kidogo; Mungu Mwenye Uwezo hawezi kufanya kosa.

11 Mungu atamulipa mutu kadiri ya matendo yake, atamulipiza kulingana na mwenendo wake.

12 Ni ukweli mutupu: Mungu hafanyi jambo ovu. Mungu Mwenye Uwezo hapotoshi haki hata kidogo.

13 Kuna yule aliyemupatia mamlaka juu ya dunia? Uwezo wake juu ya ulimwengu ni wake peke yake.

14 Kama Mungu angejifikiri tu yeye mwenyewe, akiondoa pumzi yake ya uzima katika dunia,

15 viumbe vyote vingeangamia kabisa, naye mwanadamu angerudi katika mavumbi.

16 Kama una akili sikiliza; sikiliza ninachokuambia.

17 Anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki? Utasubutu kumuhukumu mwenye haki na mwenye nguvu,

18 anayemwambia mufalme “Wewe ni wa ovyo!” na watu wenye heshima “Ninyi ni waovu!”

19 Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.

20 Kufumba na kufumbua hao wamekufa; wanatikiswa usiku na kuaga dunia; nao wenye nguvu wanaondolewa bila kutumia nguvu za mutu.

21 Macho ya Mungu yanachunguza mienendo ya watu; yeye anaziona hatua zao zote.

22 Hakuna weusi wala giza kubwa ambamo watenda maovu wanaweza kujificha.

23 Mungu hahitaji kumujulisha mutu wakati wa kumuleta mbele ya tribinali yake.

24 Anawaangamiza wenye nguvu bila uchunguzi, na kuwaweka wengine pahali pao.

25 Kwa maana anayajua matendo yao yote, anawapindua usiku waangamie.

26 Anawapiga mbele ya watu kwa ajili ya uovu wao,

27 kwa sababu wameacha kumufuata yeye, wakazarau njia zake zote.

28 Hata wakasababisha kilio cha wamasikini kimufikie Mungu. Mungu akasikiliza kilio cha wale walioteswa.

29 Kama Mungu akinyamaza, nani anayeweza kumuhukumu? Kama akificha uso wake, nani anayeweza kumwona, ikiwa ni taifa au mutu mumoja?

30 Anafanya hivyo, mutu mubaya asitawale, au wale wanaohatarisha maisha ya watu.

31 Labda mutu atamwambia Mungu hivi: “Nimekosa, sitatenda zambi tena.

32 Unionyeshe makosa nisiyoweza kuyaona. Kama nimetenda mabaya, sitayarudilia tena.”

33 Mungu atapaswa kumwazibu kama unavyoona wewe? Wewe ndiwe unayeamua, wala si mimi. Basi, sema unachofikiri wewe.

34 Mutu yeyote mwenye akili, na kila mwenye hekima anayenisikiliza atasema:

35 “Yobu anaongea bila kutumia akili, maneno yake hayana maana.”

36 Heri Yobu angechunguzwa mpaka mwisho, kwa maana anajibu kama watu waovu.

37 Anaongeza uasi juu ya zambi zake; anaeneza mashaka kati yetu, na kuzidisha maneno yake juu ya Mungu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan