Yobu 29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Kisha Yobu akaendelea na masemi yake, akasema: 2 Heri ningekuwa kama zamani, wakati ule ambapo Mungu alinichunga, 3 wakati taa yake iliponiangazia juu ya kichwa, na kwa mwangaza wake nilitembea katika giza. 4 Wakati ule nilifikia ukamilifu wa maisha, wakati urafiki wa Mungu ulikaa ndani ya nyumba yangu. 5 Mungu Mwenye Uwezo alikuwa angali pamoja nami, na watoto wangu walinizunguka. 6 Nyakati hizo niliogelea kwenye fanaka. Mawe yalinitiririshia vijito vya mafuta. 7 Nilipokutana na wazee kwenye mulango wa muji na kutwaa nafasi yangu katika mukutano, 8 vijana waliponiona walisimama pembeni, na wazee walisimama wima kwa heshima. 9 Wakubwa waliponiona waliacha kuzungumuza, waliweka kidole juu ya midomo kuwaomba watu wakae kimya. 10 Sauti za waheshimiwa zilinyamazishwa, na vinywa vyao vikafumbwa. 11 Kila mutu aliyesikia habari zangu alinitakia heri na aliponiona, alikubali habari zile kuwa kweli. 12 Nilimwokoa masikini aliyenililia kupata musaada, vilevile na yatima asiyekuwa na wa kumusaidia. 13 Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka. Niliwafanya wajane waone tena furaha ndani ya moyo. 14 Haki ilikuwa ndiyo nguo yangu; kufuata sheria ya Mungu kulikuwa kama vile kanzu na taji langu. 15 Kwa vipofu nilikuwa macho ya kuwaonyesha njia; kwa viwete nilikuwa miguu yao. 16 Kwa wamasikini nilikuwa baba yao; nilifanya bidii kutetea haki za watu nisiowajua. 17 Nilivunja nguvu za watu waovu, nikawafanya wawaachilie mateka wao. 18 Kisha nikafikiri: “Nitakufia ndani ya chicha yangu,” na siku za maisha yangu zitaongezeka kama vile muchanga. 19 Mimi ni kama vile muti uliotandaza mizizi ndani ya maji; umande wa usiku unanyesha juu ya matawi yangu. 20 Ninapata utukufu mupya siku zote, na nguvu zangu tayari kama vile mushale na upinde. 21 Wakati ule watu walinisikiliza na kungoja, walikaa kimya kungojea mashauri yangu. 22 Nilipomaliza kusema hawakukuwa na cha kuongeza; maneno yangu yaliwakolea kama vile matone ya mvua. 23 Watu waliningojea kama vile wanavyongojea mvua, walikuwa kama vile watu wanaotazamia mvua ya kwanza. 24 Walipokata tamaa, niliwaonyesha uso wa furaha; walishika muchangamuko wa uso wangu. 25 Niliwatangulia kwa kuwaongoza, nikawaonyesha njia. Nilikuwa kwao kama vile mufalme kati ya majeshi yake; kama vile mutu anayewafariji wenye musiba. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo