Yobu 25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Kisha Bildadi wa inchi ya Suhi akajibu: 2 Mungu ni mwenye uwezo mukubwa, watu wote wamwogope. Yeye anaweka amani mpaka juu kwake mbinguni. 3 Nani anayeweza kuhesabu majeshi yake? Ni nani asiyeangaziwa na mwangaza wake? 4 Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi? 5 Kwake Mungu, hata mwezi hauangai vya kutosha, nyota nazo si safi mbele yake; 6 ni nini sasa mutu ambaye ni kidudu, mwanadamu ambaye ni nondo tu! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo