Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Yobu akajibu:

2 Hata leo malalamiko yangu ni ya uchungu. Ninapata maumivu na kuugua.

3 Heri ningejua pahali nitakapomupata Mungu! Ningeweza kwenda hata karibu naye.

4 Ningeleta maneno yangu mbele yake, na kumutolea utetezi wangu.

5 Ningeweza kujua atakachonijibu, na kuelewa atakachoniambia.

6 Angeshindana nami kwa nguvu zake zote? Hapana! Bila shaka angenisikiliza.

7 Pale, mutu wa usawa anaweza kujitetea. Mungu, mwamuzi wangu angeamua kuwa sina kosa milele.

8 Ninakwenda mbele, lakini simupati; ninarudi nyuma, lakini siwezi kumwona.

9 Ninamutafuta upande wa kushoto lakini simwoni; ninageukia upande wa kuume, lakini siwezi kumwona.

10 Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.

11 Ninamufuata kabisa; njia yake nimeishikilia wala sikugeuka pembeni.

12 Sijaacha hata kidogo kushika amri yake; maneno yake nimeyatunza ndani ya moyo wangu.

13 Lakini yeye habadiliki, nani anayeweza kumugeuza? Kitu anachotaka, ndicho anachofanya!

14 Anatimiza yote aliyonipangia; na mengi kama hayo yako katika akili yake.

15 Kwa hivyo, ninatetemeka kwa hofu mbele yake; hata nikifikiri tu ninapatwa na woga.

16 Mungu amefanya moyo wangu uregee, Mungu Mwenye Uwezo amenitia hofu.

17 Maana nimepatwa na giza, na giza kubwa limetanda katika uso wangu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan