Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yobu 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Yobu akajibu:

2 Mutaendelea kunitesa mpaka wakati gani, na kunivunjavunja kwa maneno?

3 Mara hizi zote kumi mumenitukana. Basi, hamusikii haya kunitendea vibaya?

4 Hata kama ingekuwa nimekosa kweli, kosa langu linanielekea mimi mwenyewe.

5 Munaishusha hali yangu mupate kujipandisha; munanitusi kwa kunyenyekezwa kwangu.

6 Mujue kwamba Mungu amenitendea vibaya na kuninasa katika wavu wake.

7 Ninalalamika: “Mateso makali!” lakini sijibiwi. Ninaita kwa sauti kubwa, lakini sipati haki yangu.

8 Njia yangu ameiziba kwa ukuta kusudi nisipite, njia zangu amezitia giza.

9 Amenivua utukufu wangu; ameiondoa taji yangu juu ya kichwa.

10 Amenivunja pande zote, nami nimekwisha; tumaini langu ameliongoa kama muti.

11 Ameichochea kasirani yake juu yangu; ameniona kuwa kama adui yake.

12 Majeshi yake yananifikia kwa pamoja; yametengeneza njia ya kuja kwangu, yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.

13 Mungu amewaweka wandugu zangu mbali nami; warafiki zangu wakubwa wamenitoroka kabisa.

14 Wandugu zangu na warafiki hawanisaidii tena.

15 Wageni katika nyumba yangu wamenisahau; wajakazi wangu wananiona kuwa mugeni. Mimi nimekuwa kwao mutu wasiyemujua.

16 Ninamwita mutumishi wangu lakini haitikii, ninalazimishwa kumusihi sana kwa maneno.

17 Nimekuwa harufu mbaya kwa muke wangu; chukizo kwa wandugu zangu wa tumbo.

18 Hata watoto wadogo wananizarau; wakati ninapojitokeza wao wananizomea.

19 Warafiki zangu wakubwa wanachukizwa nami, wale niliokuwa nikiwapenda wamenigeuka.

20 Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi, nimeponyoka kisha kupoteza yote.

21 Munionee huruma, munionee huruma, enyi warafiki zangu; maana mukono wa Mungu umenigusa.

22 Kwa nini munanifuatilia kama Mungu? Mbona hamutosheki na mwili wangu?

23 Heri maneno yangu yangeandikwa! Heri yangeandikwa katika kitabu!

24 Heri yangechorwa kwa chuma na risasi juu ya jiwe kusudi yadumu!

25 Ninajua wazi Mukombozi wangu anaishi. Kwa mwisho yeye atasimama hapahapa katika dunia.

26 Na nyuma ngozi yangu kuharibika hivyo, nitamwona Mungu nikiwa na mwili huu.

27 Mimi mwenyewe nitakutana naye. Mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho. Moyo wangu unachomwa kwa kumungojea.

28 Ninyi munaweza kujisemesha: “Tutamufuatilia namna gani? Namna gani tutapata kwake maneno ya kumushitaki?”

29 Lakini muogope azabu, chuki yenu isiwaletee kifo. Mujue kwamba kutakuwa hukumu!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan