Yobu 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Mutu anazaliwa na mwanamuke, ana siku chache, na taabu nyingi. 2 Anachanua kama maua, kisha ananyauka. Anakimbia kama kivuli na kutoweka. 3 Ee Mungu, kwa nini unajali hata kumwangalia na kuanza kusamba naye? 4 Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza. 5 Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa. Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake; hawezi kupita mupaka uliomwekea. 6 Angalia pembeni basi, umwache, kusudi apate kufurahia siku zake kama mutumishi wa mushahara. 7 Muti ukikatwa, kuna tumaini la kuota, unaweza kuchipuka tena. 8 Japo mizizi yake itazeeka katika udongo, na shina lake kukufia ndani ya udongo, 9 lakini kwa harufu tu ya maji utachipuka, utatoa matawi kama chipukizi. 10 Lakini mutu anakufa na ule ndio mwisho wake. Akisha kutoa roho, anabakiliwa na nini tena? 11 Kama vile maji yanavyokauka katika ziwa, na muto unavyokoma kutiririka, 12 ndivyo mutu anavyokufa, wala haamuki tena. Hataamuka tena wala kusisimuka, hata pale mbingu zitakapotoweka. 13 Heri ungenificha katika kuzimu, ungenificha mpaka kasirani yako itulie, nawe ungenipimia muda kwa kunikumbuka tena. 14 Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike. 15 Halafu ungeniita, nami ningeitika, wakati ungetaka kuniona mimi kiumbe chako. 16 Kwa hiyo ungeweza kuhesabu hatua zangu, ungeacha kuchunguza zambi zangu. 17 Makosa yangu yangefungiwa katika mufuko, nawe ungefunika uovu wangu. 18 Lakini milima inaanguka nayo mawe yanaongoka pahali pake. 19 Mitiririko wa maji inakulakula mawe, mvua kubwa inaleta mumomonyoko wa udongo. Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la mwanadamu. 20 Wewe unamwangusha mwanadamu, naye anatoweka milele; unaubadilisha uso wake na kumutupilia mbali. 21 Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari. Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa. 22 Anasikia tu maumivu ya mwili wake, na kuomboleza tu hali yake mbaya. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo