Yobu 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Kisha Zofari wa inchi ya Namati akamujibu Yobu: 2 Wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa? Mutu wa maneno mengi anaonyesha kwamba hana kosa? 3 Kupapayuka kwako kutanyamazisha watu? Kama ukichekelea watu, hakuna atakayekupatisha haya? 4 Wewe unasema: “Masemi yangu ni safi, mimi sina kosa mbele ya Mungu.” 5 Heri Mungu angefungua kinywa chake na kutoa sauti yake kwa kukujibu! 6 Angekuelezea siri za hekima, maana yeye yuko na maarifa mengi. Ujue kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote. 7 Unaweza kuvumbua siri za Mungu na kujua ukomo wa Mungu Mwenye Uwezo? 8 Ukubwa wake unapita mbingu; wewe unaweza nini? Kimo chake kinapita kuzimu; wewe unaweza kujua nini? 9 Ukubwa ule unapita urefu wa dunia, unapita upana wa bahari. 10 Kama Mungu akipita, akimufunga mutu na kumuhukumu, nani anayeweza kumuzuia? 11 Mungu anajua watu wasiofaa; anaona uovu vilevile bila magumu. 12 Mupumbafu hawezi kuwa na maarifa. Punda wa pori ni punda wa pori tu. 13 Yobu, ukifanya moyo wako mukamilifu, utainua mikono yako kwa kumwomba Mungu! 14 Kama uovu uko katika mukono wako, uutupilie mbali. Usikubali ubaya ukuwe katika nyumba yako. 15 Halafu utainua uso wako bila kosa, utakuwa imara bila kuwa na hofu. 16 Utazisahau taabu zako zote; utazikumbuka tu kama mafuriko yaliyopita. 17 Maisha yako yataangaa kuliko jua la muchana kati, giza lake litabadilika kuwa mapambazuko. 18 Utakuwa na uhakika maana kuna tumaini; utalindwa na kupumzika salama. 19 Utalala bila kuogopeshwa na mutu; watu wengi watakuomba musaada. 20 Lakini waovu macho yao yatafifia, njia zote za kutorokea zitawapotea; tumaini lao la mwisho ni kukata roho! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo