Yobu 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Ninachukia maisha yangu! Malalamiko yangu nitayasema bila kizuizi. Nitasema kwa uchungu wa moyo wangu. 2 Nitamwambia Mungu: Usinitendee sawa na mwenye makosa. Unijulishe sababu ya kugombana nami. 3 Ni sawa kwako kunionea, kuzarau kazi ya mikono yako na kupendelea mipango ya waovu? 4 Uko na macho kama ya mwanadamu? Unaona kama vile mwanadamu anavyoona? 5 Siku zako ni kama za mwanadamu? Miaka yako kama ya mwanadamu? 6 Kwa nini unachunguza uovu wangu na kuitafuta zambi yangu? 7 Wewe unajua kwamba mimi sina kosa, na hakuna wa kuniokoa toka katika mikono yako. 8 Mikono yako ilinitengeneza na kuniumba, lakini sasa unageuka kwa kuniangamiza. 9 Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Utanirudisha tena katika mavumbi? 10 Si wewe uliyenimimia kama maziwa, na kunigandisha kama siagi? 11 Uliuumba mwili wangu kwa mifupa na mishipa, ukaifunika mifupa yangu kwa nyama na ngozi. 12 Ukanipa uzima na kunitendea mema, ukalinda nafsi yangu kwa uangalifu. 13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha ndani ya moyo. Lakini ninajua kwamba ile ilikuwa nia yako. 14 Ulikuwa unangojea uone kama nitatenda zambi, kusudi ukatae kunisamehe uovu wangu. 15 Kama mimi ni mwovu, ole wangu! Kama mimi ni mwenye haki, siwezi kujisifu; maana nimejaa haya, nikiangalia mateso yangu. 16 Nikiinua kichwa tu, unaniwinda kama simba na kuniponda tena kwa maajabu yako. 17 Kila mara uko na ushuhuda juu yangu, unaongeza hasira yako juu yangu, unaniletea waadui wapya wanishambulie. 18 Ee Mungu, kwa nini ulinitoa katika tumbo ya mama? Afazali ningekufa mbele ya watu kuniona, 19 ningepelekwa katika kaburi, na kuwa kama mutu asiyekuwa. 20 Siku za maisha yangu si chache? Uniachilie nipate kufurahi kidogo, 21 mbele ya kwenda kule ambako sitarudi, kule kwenye inchi ya huzuni na giza kubwa; 22 inchi ya huzuni na fujo, ambako mwangaza wake ni kama giza. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo