Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yoane 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Yesu anawatokea wanafunzi wake saba

1 Nyuma ya mambo hayo, Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kandokando ya ziwa la Tiberia. Angalia sasa namna alivyowatokea:

2 Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.

3 Simoni Petro akawaambia wenzake hivi: “Ninakwenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia: “Na sisi vilevile tutakwenda pamoja nawe.” Basi wakaondoka, wakaingia katika chombo. Usiku ule hawakupata kitu.

4 Asubui mapema, Yesu akaonekana kandokando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakutambua kwamba ni yeye.

5 Basi Yesu akawauliza: “Watoto wangu, mumepata samaki?” Wakamujibu: “Hapana.”

6 Yeye akawaambia: “Mutupe wavu upande wa kuume wa chombo na mutapata samaki.” Basi wakatupa wavu, nao wakashindwa kuukokota, kwa sababu ulikuwa umejaa samaki wengi.

7 Halafu mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu akamwambia Petro: “Ni Bwana.” Simoni Petro aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa kanzu yake (kwa maana alikuwa havai kitu), naye akajitupa ndani ya maji.

8 Wanafunzi wengine wakakuja katika chombo wakikokota wavu uliojaa samaki. Nao hawakukuwa mbali kabisa na inchi kavu, iliwabakilia yapata metre mia moja tu.

9 Walipofika inchi kavu wakaona mukate na samaki zinazokuwa juu ya moto.

10 Yesu akawaambia: “Mulete sehemu ya samaki munaotoka kuvua.”

11 Basi Simoni Petro akapanda ndani ya chombo, akakokota wavu mpaka inchi kavu. Nao ulikuwa umejaa samaki wakubwa mia moja makumi tano na tatu. Na ijapokuwa walikuwa wengi vile, wavu haukupasuka.

12 Yesu akawaambia: “Mukuje mukule.” Na hakuna hata mumoja kati ya wanafunzi aliyesubutu kumwuliza kwamba yeye ni nani, kwa maana walijua kwamba ni Bwana.

13 Basi Yesu akawajongelea, akatwaa mukate, akawagawanyia; na kuwapa samaki vilevile.

14 Hii ndiyo mara ya tatu Yesu aliyowatokea wanafunzi wake tangu alipofufuka.


Yesu na Petro

15 Walipokwisha kula, Yesu akamwuliza Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda mimi kuliko hawa?” Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza wana-kondoo wangu.”

16 Akamwuliza tena mara ya pili: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia tena: “Chunga kondoo wangu.”

17 Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.

18 Ninakuambia mambo ya kweli: wakati ulipokuwa kijana, ulijivalisha wewe mwenyewe na kwenda pahali ulipotaka. Lakini wakati utakapokuwa muzee, utanyoosha mikono yako na mutu mwingine atakuvalisha na kukupeleka pahali usipotaka.”

19 (Yesu alisema maneno haya kwa kuonyesha kifo gani Petro atakachokufa na kumutukuza Mungu.) Kisha kusema maneno haya, Yesu akamwambia: “Unifuate!”


Yesu na mwanafunzi mupendwa

20 Petro akageuka, akaona nyuma yao mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu. (Ni yeye aliyeegamia kifua cha Yesu wakati wa chakula na kumwuliza: “Bwana, ni nani yule atakayekutoa?”)

21 Basi wakati Petro alipomwona, akamwuliza Yesu: “Bwana, na mutu huyu, ni nini itakayomufikia?”

22 Yesu akamujibu: “Ikiwa ninataka huyu aishi mpaka nitakaporudi, jambo hili halikuangalii! Wewe, unifuate!”

23 Basi habari hii ikaenea kati ya wandugu waamini wa Yesu kwamba yule mwanafunzi hatakufa. Yesu hakusema kama hatakufa; lakini alisema: “Ikiwa ninataka huyu aishi mpaka nitakapokuja, jambo hili halikuangalii.”

24 Ni huyu huyu mwanafunzi ndiye aliyeshuhudia mambo hayo na kuyaandika; nasi tunajua kwamba ushuhuda wake ni wa kweli.


Maneno ya mwisho

25 Kuna mambo mengine mengi Yesu aliyofanya. Lakini yote yangeandikwa moja kwa moja, ninazani hata dunia nzima haingetosha kwa kuwekea vitabu ambavyo vingeandikwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan