Yoane 17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi ya Yesu 1 Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile. 2 Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa. 3 Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma. 4 Mimi nimekutukuza wewe katika dunia kwa kuwa nimemaliza kazi ile uliyonipa. 5 Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia. 6 “Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako. 7 Sasa wanajua kwamba yote uliyonipa yanatoka kwako; 8 kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 9 “Ninawaombea wao; siwaombei watu wa dunia, lakini hao ulionipa, kwa sababu wao ni wako. 10 Na yote ninayokuwa nayo ni yako, na yote unayokuwa nayo ni yangu, nami nimetukuzwa kwa njia yao. 11 Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja. 12 Wakati nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda kwa uwezo wa jina lako, ndilo lile jina ulilonipa. Nimewachunga wala hakuna mumoja wao aliyepotea, isipokuwa yule anayepaswa kupotea, kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe. 13 Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao. 14 Mimi nimetangaza neno lako kwao, na dunia imewachukia kwa sababu wao si wa dunia, kama vile mimi nisivyokuwa wa dunia. 15 Sikuombi kama uwaondoe katika dunia, lakini ninakuomba uwakinge na yule Mwovu Shetani. 16 Wao si wa dunia, kama vile mimi nisivyokuwa wa dunia. 17 Uwatakase wapate kujitoa kwako kabisa kwa njia ya ukweli, maana yake kwa njia ya neno lako la kweli. 18 Kama vile ulivyonituma katika dunia, mimi vilevile nimewatuma katika dunia. 19 Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa. 20 “Siwaombei hawa tu, lakini ninawaombea vilevile wale watakaoamini kwa sababu ya mafundisho yao. 21 Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma. 22 Nami nimewapa utukufu ulionipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja. 23 Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda. 24 “Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia. 25 Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma. 26 Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo