Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yoane 16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 “Nimewaambia maneno hayo, kusudi musikwazwe katika imani yenu.

2 Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.

3 Watafanya hivi kwa sababu hawakumujua Baba wala mimi.

4 Lakini ninawaambia maneno haya kusudi wakati ule utakapotimia mupate kukumbuka kwamba nimekwisha kuwaambia. “Sikuwaambia ninyi maneno hayo mbele kwa sababu nilikuwa ningali pamoja nanyi.


Kazi ya Roho Mutakatifu

5 Sasa ninarudi kwake yule aliyenituma na hakuna mumoja wenu anayeniuliza kwamba ninaenda wapi.

6 Lakini kwa sababu nimewaambia maneno haya, mumesikitika sana.

7 Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.

8 Naye atakapokuja, atahakikisha watu wa dunia hii juu ya zambi zao, juu ya haki yangu, na juu ya hukumu ya Mungu.

9 Kuelekea zambi ni kwa sababu hawaniamini mimi.

10 Kuelekea haki ni kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamutaniona tena.

11 Na kuelekea hukumu ni kwa sababu mutawala wa dunia hii amekwisha kuhukumiwa.

12 “Ningali na maneno mengi ya kuwaambia, lakini sasa hamujakuwa na uwezo wa kuyafahamu.

13 Lakini wakati yule Roho wa ukweli atakapokuja, atawaongoza ninyi kufuata ukweli wote kabisa. Yeye hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, lakini atasema tu yale atakayosikia, naye atawatangazia ninyi habari za mambo yatakayokuja.

14 Yeye atanitukuza mimi kwa sababu maneno atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.

15 Yote Baba anayokuwa nayo ni yangu. Ni kwa sababu hii nilisema kwamba maneno Roho atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.


Huzuni na furaha

16 “Kunabaki wakati kidogo, ninyi hamutaniona; lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena.”

17 Basi wanafunzi wake wamoja wakasemezana hivi: “Yeye anatuambia kwamba kunabakia wakati kidogo nasi hatutamwona, lakini kisha wakati kidogo tutamwona tena. Vilevile anasema kwamba ni kwa sababu anakwenda kwa Baba yake. Maana ya maneno haya yote ni nini?”

18 Nao wakaendelea kuulizana: “Maana ya ‘wakati kidogo’ ni nini? Hatufahamu nini anayosema.”

19 Yesu alitambua kwamba walitaka kumwuliza. Basi akawaambia: “Munaulizana juu ya maneno niliyosema kwamba kunabaki wakati kidogo nanyi hamutaniona, lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena?

20 Kweli, kweli ninawaambia: mutalia na kusikitika, lakini watu wa dunia watafurahi. Mutahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.

21 Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.

22 Na sasa ninyi vilevile munasikia uchungu, lakini nitawaona tena, nanyi mutafurahi, wala hakuna mutu atakayeweza kuwahuzunisha tena.

23 “Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.

24 Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Yesu ni mushindaji wa dunia

25 “Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.

26 Siku ile itakapotimia, mutamwomba Baba kwa jina langu. Mimi sisemi kwamba nitawaombea ninyi kwa Baba,

27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda. Anawapenda ninyi kwa sababu mumenipenda na kuamini kwamba nilitoka kwa Mungu.

28 Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”

29 Basi wanafunzi wake wakamwambia: “Sasa unasema waziwazi pasipo kutumia mifano.

30 Sasa tunajua kwamba unajua yote na si lazima mutu akuulize kitu. Sababu hii tunaamini kama ulitoka kwa Mungu.”

31 Yesu akawauliza: “Munaamini sasa?

32 Kutakuwa wakati, nao umetimia, ndio wakati mutakaposambazwa, kila mutu akijiendea ngambo yake mwenyewe, nanyi mutaniacha peke yangu. Lakini mimi si peke yangu kabisa, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.

33 Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan