Yoane 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Neno aliyefanyika kuwa mutu 1 Kwa mwanzo, Neno alikuwa yuko, naye Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. 2 Kwa mwanzo Neno alikuwa pamoja na Mungu. 3 Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye. 4 Yeye alikuwa chemichemi ya uzima, na uzima huu ulikuwa mwangaza kwa watu. 5 Mwangaza ule uliangaza katika giza, wala giza halikuuzimisha. 6 Kulitokea mutu aliyetumwa na Mungu, jina lake Yoane. 7 Alikuja kushuhudia ule mwangaza kusudi watu wote wapate kuamini kwa njia yake. 8 Yeye mwenyewe hakukuwa mwangaza ule, lakini alikuja tu kuushuhudia. 9 Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia. 10 Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua. 11 Alikuja katika inchi yake, lakini taifa lake halikumupokea. 12 Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu. 13 Hawakuzaliwa kuwa watoto wa Mungu kwa namna ya kimutu, wala kwa mapenzi ya kimwili, wala kwa mapenzi ya mutu, lakini wamezaliwa na Mungu. 14 Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba. 15 Yoane alimushuhudia akisema kwa sauti: “Huyu ndiye niliyesema juu yake: ‘Anayekuja nyuma yangu ananipita, kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.’ ” 16 Sisi wote tumepokea sehemu ya neema aliyojaa nayo, akitupatia baraka nyingi sana. 17 Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo. 18 Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu. Ushuhuda wa Yoane Mubatizaji ( Mat 3.1-12 ; Mk 1.1-8 ; Lk 3.1-18 ) 19 Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani. 20 Yoane aliwajibu hivi waziwazi bila kukana: “Mimi si Kristo.” 21 Halafu wakamwuliza: “Basi wewe ni nani? Wewe ni Elia?” Yoane akajibu: “Mimi si yeye.” Wakamwuliza tena: “Wewe ni yule nabii?” Naye akawajibu: “Hapana.” 22 Basi wakamwambia: “Wewe ni nani? Utuambie kusudi tuende kuwaelezea wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?” 23 Yoane akajibu: “Mimi ni sauti inayotangaza katika jangwa: ‘Munyooshe njia ya Bwana,’ ” sawa vile nabii Isaya alivyosema. 24 Nao wale waliotumwa walikuwa Wafarisayo. 25 Wakamwuliza Yoane: “Ikiwa wewe si Kristo, wala Elia, wala yule nabii, basi sababu gani unabatiza?” 26 Yoane akawajibu: “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini kati yenu kuna mutu ninyi musiyemujua, 27 anayekuja nyuma yangu. Mimi sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.” 28 Mambo hayo yalifanyika Betania, ngambo ya muto Yordani, pahali Yoane alipokuwa akibatiza. Yesu Mwana-Kondoo wa Mungu 29 Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia! 30 Huyu ndiye niliyesema juu yake kwamba mutu mumoja anakuja nyuma yangu, lakini ananipita kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa. 31 Mimi sikumujua, lakini nimekuja kubatiza kwa maji kusudi ajulikane kwa taifa la Waisraeli.” 32 Yoane akatoa ushuhuda huu: “Nimemwona Roho akishuka juu yake toka mbinguni kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake. 33 Mimi sikumujua ni nani, lakini yule aliyenituma kubatiza kwa maji aliniambia: ‘Yule utakayemwona Roho akishuka juu yake na kukaa juu yake, mutu yule ndiye anayebatiza kwa Roho Mutakatifu.’ 34 Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.” Wanafunzi wa kwanza wa Yesu 35 Kesho yake Yoane alikuwa pale tena pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake. 36 Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.” 37 Wale wanafunzi wawili waliposikia maneno yale, wakamufuata Yesu. 38 Yesu akageuka, akawaona wakimufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakajibu: “Rabi (maana yake ‘Mwalimu’), unakaa wapi?” 39 Naye akawajibu: “Mukuje na mutaona.” Basi wakaenda, wakaona pahali alipokaa, wakabaki pamoja naye siku ile. (Ilikuwa karibu na saa kumi ya magaribi.) 40 Andrea, ndugu ya Simoni Petro, alikuwa mumoja wa wale wawili waliosikia maneno ya Yoane na kumufuata Yesu. 41 Andrea alimukuta kwanza Simoni, ndugu yake wa tumbo na kumwambia: “Tumemwona Masiya” (maana yake “Kristo”). 42 Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”) Filipo na Natanaeli wanaitwa kumufuata Yesu 43 Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Alipomukuta Filipo akamwambia: “Unifuate.” 44 (Filipo alikuwa muzaliwa wa Betesaida, muji wa Andrea na Petro.) 45 Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.” 46 Natanaeli akamwuliza: “Kuna kitu kizuri kinachoweza kutoka Nazareti?” Filipo akamujibu: “Kuja uone.” 47 Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!” 48 Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.” 49 Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.” 50 Yesu akamujibu: “Unaamini kwa sababu nimekuambia kama nilikuona chini ya muti wa tini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.” 51 Yesu akaongeza kumwambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: mutaona mbingu zimefunguka na wamalaika wa Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwenye Mwana wa Mutu!” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo