Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yeremia 43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Yeremia anapelekwa Misri

1 Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno yote ambayo Yawe, Mungu wao, alimwamuru awatangazie,

2 Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.

3 Baruku mwana wa Neria, amekuchochea juu yetu kusudi tutiwe katika mikono ya Wakaldea watuue au watupeleke katika uhamisho kule Babeli.

4 Basi, Yohana mwana wa Karea na wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wote hawakutii maneno ya Yawe, kwamba wabaki katika inchi ya Yuda.

5 Halafu Yohana mwana wa Karea na wakubwa wote wa waaskari waliwapeleka watu wote wa Yuda waliobaki ambao walikuwa wamerudi katika inchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wamesambazwa:

6 wanaume, wanawake, watoto, wabinti wa mufalme na kila mutu ambaye Nebuzaradani mukubwa wa waaskari alikuwa amemwachia Gedalia mwana wa Ahikamu mujukuu wa Safanu. Wakamupeleka vilevile nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria.

7 Wakaenda katika inchi ya Misri, wakafika katika muji wa Tapanesi. Ndivyo walivyokataa kutii maneno ya Yawe.

8 Wakati Yeremia alipokuwa Tapanesi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:

9 Twaa mawe makubwa, uyafiche ndani ya udongo kwenye matofali mbele ya mulango wa nyumba ya kifalme ya Tapanesi mbele ya Wayuda.

10 Kisha uwaambie hivi: Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Muangalie, mimi nitamutuma na kumuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mutumishi wangu, naye ataweka kiti chake cha kifalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha hapa, na kutandaza paa la kifalme juu yake.

11 Atakapofika ataiangamiza inchi ya Misri. Kwa hiyo waliopangiwa kufa kwa ugonjwa watakufa kwa ugonjwa, waliopangiwa kukamatwa mateka, watakamatwa mateka; waliopangiwa kufa kwa vita watakufia katika vita.

12 Mimi nitawasha moto katika mahekalu ya miungu ya Misri; naye Nebukadneza ataiteketeza miungu hiyo kwa moto au kuikamata mateka mpaka Babeli. Ataisafisha inchi ya Misri kama muchungaji anavyoondoa vidudu katika nguo yake na kuondoka Misri akiwa mushindi.

13 Ataivunja minara ya mungu wao inayokuwa huko Heliopoli katika inchi ya Misri, na atateketeza mahekalu ya miungu ya Misri kwa moto.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan