Yeremia 39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kutekwa kwa Yerusalema 1 Katika mwezi wa kenda wa mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia mufalme wa Yuda, Nebukadneza mufalme wa Babeli alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, akauzunguka kwa vita. 2 Na katika siku ya kenda ya mwezi wa ine, mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Zedekia, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa. 3 (Basi wakubwa hawa wote wa mufalme wa Babeli waliingia na kukaa kwenye mulango wa katikati: Nergali-Sarezeri, Samgari-Nebo, Sarsekimu jemadari mukubwa wa na Nergali-Sarezeri mukubwa wenye maarifa, pamoja na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babeli.) 4 Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani. 5 Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu. 6 Kulekule Ribla, mufalme wa Babeli aliwaua wana wa Zedekia mbele ya baba yao. Waliwaua vilevile wakubwa wote wa Yuda. 7 Kisha aliongoa macho ya Zedekia na kumufunga kwa minyororo, kusudi amupeleke Babeli. 8 Wakaldea waliichoma kwa moto nyumba ya kifalme na nyumba za watu; vilevile walizibomoa kuta za Yerusalema. 9 Kisha, Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho kule Babeli watu waliokuwa wamebaki katika muji na wale waliokuwa wamejitoa kwake pamoja na wafundi wote waliokuwa wamebaki. 10 Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwaacha katika inchi ya Yuda watu wamoja wamasikini ambao hawakukuwa na kitu chochote, akawagawanyia mashamba ya mizabibu na kuwapa maeneo ya kulima wakati huohuo. Yeremia anafunguliwa 11 Nebukadneza mufalme wa Babeli alikuwa amemupa Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, amri hii juu ya Yeremia: 12 Umutwae Yeremia, umutunze vema wala usimuzuru; umutendee kama anavyokuambia. 13 Basi, Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, Nebusazibani, Nergali-Sarezeri pamoja na wakubwa wote wa mufalme wa Babeli, wakatuma watu wamwondoe Yeremia katika chumba cha walinzi. 14 Wakamutoa Yeremia kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, amupeleke katika nyumba yake. Basi, Yeremia akaishi pamoja na wanainchi wengine. Tumaini la Ebedimeleki 15 Wakati Yeremia alipokuwa amefungwa katika chumba cha walinzi, neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: 16 Kwenda kwa Ebedimeleki Mwetiopia umwambie hivi: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Angalia mimi nitatimiza mambo yale niliyosema juu ya muji huo na sio mambo mema. Mambo hayo yatakamilika siku hiyo ukiona wewe mwenyewe. 17 Lakini siku hiyo mimi nitakuokoa wewe, wala hautatiwa katika mikono ya watu unaowaogopa. 18 Maana, kweli nitakuokoa na hautauawa kwa vita; utapata faida ya kuokoa maisha yako kwa sababu umeniamini mimi. –Ni ujumbe wa Yawe. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo