Yeremia 28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Yeremia na nabii Hanania 1 Katika mwaka uleule, maana yake mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Zedekia juu ya Yuda, katika mwezi wa tano, Hanania, mwana wa Azuri, nabii kutoka muji Gibeoni, alisema nami katika nyumba ya Yawe. Alisema nami mbele ya makuhani na watu wote, akiniambia kwamba 2 Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimevunja nira mufalme wa Babeli anayowabebesha. 3 Mbele ya miaka miwili nitavirudisha hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yawe ambavyo Nebukadneza, mufalme wa Babeli alivikamata na kuvipeleka Babeli. 4 Vilevile nitamurudisha Yekonia mwana wa Yoyakimu mufalme wa Yuda pamoja na watu wote wa Yuda waliohamishiwa Babeli. Hakika nitaivunja nira mufalme wa Babeli anayowabebesha. –Ni ujumbe wa Yawe. 5 Kisha, nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama katika hekalu la Yawe: 6 Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko. 7 Lakini sikiliza neno hili ninalokuambia wewe na watu wanaokuwa hapa: 8 Manabii waliotangulia mbele yetu, mimi na wewe, zamani za kale walitabiri kwamba vita, njaa na magonjwa makali vitazipata inchi nyingi na tawala kubwa. 9 Lakini nabii anayetabiri maneno ya amani, anaweza kutambulikana kama ni nabii aliyetumwa na Yawe, wakati mambo aliyotabiri yanapotokea. 10 Nabii Hanania akatwaa ile nira toka katika shingo la nabii Yeremia na kuivunja. 11 Naye Hanania akasema hivi mbele ya watu wote: Yawe anasema hivi: Mbele ya miaka miwili, hivi ndivyo nitakavyovunja nira ambayo mufalme Nebukadneza anayoibebesha mataifa yote. Kisha nabii Yeremia akajiendea. 12 Nyuma ya pale nabii Hanania alipovunja nira kutoka katika shingo la nabii Yeremia, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi: 13 Kwenda umwambie Hanania kwamba: Yawe anasema hivi: Wewe umevunja nira ya muti, lakini mimi nitatengeneza ingine ya chuma. 14 Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma ya utumwa kwenye shingo la mataifa yote ya pande hizi, yakuwe katika utumwa, nayo yatamutumikia Nebukadneza, mufalme wa Babeli. Nimemupa Nebukadneza hata nyama wa pori wamutumikie. 15 Basi, nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania: Sikiliza, Hanania. Yawe hakukutuma, nawe unawafanya watu hawa waamini uongo. 16 Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitakuondoa katika dunia. Mwaka huuhuu utakufa, kwa sababu umewasukuma watu wamwasi Yawe. 17 Mwaka huohuo, katika mwezi wa saba, nabii Hanania akakufa. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo