Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yeremia 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Ibada ya sanamu na ya kweli

1 Enyi Waisraeli musikilize neno Yawe analowaambia.

2 Yawe anasema hivi: Musiige mwenendo wa mataifa mengine, wala musishangazwe na vitambulisho vya ajabu munavyoviona katika mbingu; muyaache mataifa mengine yashangazwe navyo.

3 Maana, desturi za dini za watu hao ni za uongo. Kwa maana mutu anakata muti katika pori, naye fundi anachonga sanamu ya mungu kwa shoka.

4 Kisha watu wanaipamba kwa feza na zahabu wakiipigilia misumari na nyundo kusudi isianguke.

5 Sanamu zao ni kama sanamu za kutishia ndege katika shamba la maboga, hazina uwezo wa kuongea; ni lazima zibebwe maana haziwezi kutembea. Musiziogope sanamu hizo, maana haziwezi kuzuru, wala haziwezi kutenda jambo lolote jema.

6 Ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe; wewe ni mukubwa na nguvu yako inajulikana.

7 Nani asiyekuogopa wewe, ee mufalme wa mataifa? Wewe unastahili kuheshimiwa: kwa maana kati ya wenye hekima wote wa mataifa, na katika falme zao zote, hakuna hata mumoja anayekuwa kama wewe.

8 Wote ni wajinga na wapumbafu, fundisho la sanamu hizi ni mazarau matupu!

9 Sanamu hizo zinapambwa kwa feza kutoka Tarsisi, na zahabu kutoka Ofiri; zilitengenezwa na wafundi na wafua zahabu. Zimevalishwa nguo nzuri za rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi, zilizofumwa na wafundi wa kufuma.

10 Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.

11 Basi, utawaambia hivi: Miungu hiyo ambayo haikuumba mbingu na dunia itaangamia. Itatoweka kabisa toka katika dunia, hapa chini ya mbingu.


Wimbo wa kumusifu Mungu

12 Yawe aliiumba dunia kwa nguvu zake; kwa hekima yake alisimamisha ulimwengu imara, kwa akili yake alizitandika mbingu juu.

13 Anapotoa sauti, maji yananguruma katika mbingu, anapandisha mawingu toka kwa miisho ya dunia. Anaufanya umeme upige wakati wa mvua, na kuuvumisha upepo katika gala zake.

14 Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.

15 Hazina faida, ni udanganyifu mutupu; wakati zitakapoazibiwa zote zitaangamia.

16 Lakini Mungu wa Yakobo si kama sanamu hizo, maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote, na Israeli ni taifa linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Uhamisho unakaribia

17 Mufunge vitu vyenu, enyi watu muliozungukwa kwa vita.

18 Maana Yawe anasema hivi: Mara hii nitawatupa inje wakaaji wa inchi hii, nitawataabisha hata kusibaki mutu yeyote.

19 Ole wangu mimi Yerusalema, maana nimeumizwa sana! Kidonda changu ni kikubwa sana! Mimi nilikuwa nikijisemesha hivi: Hakika haya ni magumu tu, nami ninapaswa kuyavumilia.

20 Lakini hema yangu imebomolewa, kamba zake zote zimekatika; watoto wangu wameniacha, na kujiendea, wala hawako tena; hakuna wa kunisimikia tena hema yangu, wala wa kunitundikia mapazia yangu.

21 Nami Yeremia nikasema: Wachungaji wamekuwa wajinga, hawakuuliza shauri kwa Yawe; kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa, na kondoo wao wote wamesambaa.

22 Musikilize ile fujo! Angalia inakuja. Kunatokea shindo kubwa upande wa kaskazini. Taifa kutoka kaskazini linakuja kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwa, wataigeuza mapango ya mbweha!

23 Ninajua, ee Yawe, mwanadamu hana uwezo juu ya maisha yake; hakuna mutu anayeweza kuongoza maisha yake.

24 Utuonye, ee Yawe, lakini si kwa kasirani, wala kwa hasira yako, kusudi tusiangamie.

25 Umwange hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu, na juu ya watu ambao hawakutambui. Maana, wamewaua wazao wa Yakobo; wamewaua na kuwaangamiza kabisa, na inchi yao wameiacha mabomoko.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan