Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yakobo 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Upendo usiokuwa na upendeleo

1 Wandugu zangu, kufuatana na vile munavyomwamini Bwana wetu Yesu Kristo mwenye utukufu, musikuwe vilevile na upendeleo na watu.

2 Kwa mufano: tajiri mumoja anayevaa pete ya zahabu na nguo nzuri anaingia katika nyumba yenu ya kuabudia. Na kisha kunaingia vilevile masikini anayevaa nguo zinazopasukapasuka.

3 Halafu munaonyesha heshima kwa yule anayevaa vizuri na kumwambia: “Ikaa hapa kwenye nafasi nzuri.” Lakini munamwambia yule masikini: “We! Simama pale, au uikae hapa chini kwenye nafasi ya kuwekea miguu yangu.”

4 Jambo hilo halionyeshi kwamba munafanya ubaguzi, na kwamba kwa kuamua vile munaongozwa na mawazo mabaya?

5 Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.

6 Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?

7 Vilevile si wao ndio wanaotukana jina lile nzuri mulilopewa?

8 Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”

9 Lakini kama mukifanya upendeleo, munafanya zambi, nanyi munahukumiwa na Sheria kwa sababu mumeivunja.

10 Kwa maana mutu akivunja agizo moja tu la Sheria, yeye anavunja Sheria yote.

11 Kwa maana yule aliyesema “Usizini”, ndiye aliyesema vilevile “Usiue”. Basi ikiwa wewe huzini lakini unaua, wewe unavunja Sheria.

12 Basi museme na kutenda kama watu watakaohukumiwa kufuatana na sheria inayotuweka kuwa huru.

13 Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Imani na matendo

14 Wandugu zangu, ni faida gani kama mutu akisema kwamba yuko na imani lakini haionyeshi kwa njia ya matendo mazuri? Ile imani itaweza kumwokoa?

15 Kwa mufano: kaka au dada fulani akikosewa nguo au chakula,

16 itakuwa na faida gani, kama mumoja wenu anamwambia: “Mwende vizuri, mukaote moto na kushiba,” lakini hamusaidii na kitu chochote?

17 Ni hivi vilevile, imani peke yake pasipo matendo imekufa kabisa.

18 Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”

19 Si wewe unaamini kwamba kuna Mungu mumoja? Ni vizuri! Hata pepo wanaamini vile, nao wanatetemeka kwa woga.

20 Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?

21 Babu yetu Abrahamu alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo yake. Yeye alimutoa mwana wake Isaka juu ya mazabahu.

22 Basi unaona kwamba imani yake ilionekana kwa njia ya matendo yake na kwa njia hiyo ikapata kukamilishwa.

23 Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.

24 Basi munaona kwamba mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo, wala si kwa njia ya imani peke yake.

25 Ilikuwa hivi vilevile kwa yule kahaba Rahaba. Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya matendo yake, wakati alipowakaribisha wapelelezi na kuwatorosha kwa njia nyingine.

26 Kwa maana kama vile mwili usiokuwa na pumzi ndani yake umekufa, hivi vilevile imani pasipo matendo imekufa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan