Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Walawi 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Azabu kwa ajili ya maovu

1 Yawe akamwambia Musa:

2 Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yenu, akimutoa mutoto wake yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mutu huyu anapaswa kuuawa. Wanainchi wa pale watamwua kwa kumupiga mawe.

3 Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.

4 Kama wanainchi wa pahali pale hawatamwazibu mutu yule kwa kumwua,

5 mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na jamaa yake. Nitawatenga kutoka watu wao, yeye mwenyewe pamoja na wote waliokosa uaminifu kwangu kwa kumwendea mungu Moleki.

6 Kama mutu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake.

7 Kwa hiyo, mujitakase mukuwe watakatifu, maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.

8 Mushike masharti yangu na kuyatimiza. Mimi ni Yawe ninayewatakasa.

9 Mutu yeyote anayemulaani baba yake au mama yake, anapaswa kuuawa. Amemulaani baba au mama yake, kwa hiyo damu yao itakuwa juu yake mwenyewe.

10 Kama mwanaume akifanya uzinzi na muke wa mwenzake, wote wawili wanapaswa kuuawa.

11 Mwanaume akilala na mumoja wa wake za baba yake, anamupatisha baba yake haya, wote wawili wanapaswa kuuawa. Mwanaume huyo na mwanamuke huyo wote wawili watauawa na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.

12 Mwanaume yeyote akilala na muke wa mwana wake, wote wawili wanapaswa kuuawa. Wamefanya machafuko na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.

13 Kama mwanaume yeyote akilala na mwanaume mwenzake sawa vile ni mwanamuke, basi, wote wawili wanapaswa kuuawa maana wamefanya jambo linalokuwa chukizo na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.

14 Kama mwanaume akioa muke na vilevile kumwoa mama yake, huo ni uovu. Wote watatu wanapaswa kuteketezwa kwa moto maana wamefanya uovu. Mutafanya hivyo kwa kukomesha uovu kati yenu.

15 Kama mwanaume yeyote akilala na nyama anapaswa kuuawa na nyama huyo anapaswa kuuawa.

16 Kama mwanamuke anakaribia nyama na kulala naye, mwanamuke huyo anapaswa kuuawa na nyama huyo vilevile na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.

17 Kama mwanaume yeyote akimwoa dada yake, binti ya baba yake au mama yake na binti huyo akakubaliana na mwanaume huyo ambaye ni kaka yake, na kulala naye, hilo ni chukizo. Wanapaswa kutengwa na watu wao maana wamefanya jambo la haya. Huyo mwanaume atabeba lazima ya uovu wake, maana amelala na dada yake.

18 Kama mwanaume akilala na mwanamuke anayekuwa na ugonjwa wa mwezi, wote wawili wanapaswa kutengwa na watu wao; huyo mwanaume amelala na mwanamuke aliyekuwa na ugonjwa wa mwezi, na huyo mwanamuke amefunua mutiririko wa damu yake.

19 Usilale na dada ya mama yako wala na shangazi yako, maana hao ni jamaa yako wa karibu. Wote wanaotenda vile watabeba lazima ya uovu wao.

20 Kama mutu akilala na muke wa baba yake, mukubwa au mudogo, anamupatisha baba yake mukubwa au mudogo haya. Wote wawili watabeba lazima ya zambi yao. Wote wawili watakufa bila watoto.

21 Kama mwanaume akimwoa muke wa ndugu yake, anamupatisha ndugu yake haya, huo ni uchafu; wote wawili watakufa bila watoto.

22 Munapaswa kushika na kutimiza masharti yangu na maagizo yangu yote. Kama sivyo inchi ile ambamo ninawapeleka itawatapika.

23 Musifuate desturi za taifa ninalofukuza mbele yenu. Maana waliyafanya hayo yote, nami nikawachukia sana.

24 Lakini, nimekwisha kuwaambia: Mutarizi inchi yao, mimi ninawapa inchi hiyo ikuwe yenu, inchi inayotiririka maziwa na asali. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatenga na mataifa mengine.

25 Kwa hiyo, munapaswa kutia tofauti kati ya nyama asiyekuwa muchafu na anayekuwa muchafu, kati ya ndege asiyekuwa muchafu na anayekuwa muchafu. Musijichafue kwa kugusa nyama au ndege au chochote kinachotambaa juu ya udongo ambacho nimekitenga kuwa ni kichafu.

26 Kwa sababu mimi Yawe ni mutakatifu, nami nimewatenga ninyi na mataifa mengine kusudi mukuwe mali yangu, mutakuwa watakatifu.

27 Mwanaume au mwanamuke yeyote anayekuwa mulozi au muchawi, anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe. Damu yao itakuwa juu yao wenyewe.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan