Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Wakolosayi 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ninyi wabwana muwatendee watumishi wenu kwa usawa na kwa haki, mukijua kwamba ninyi vilevile muko na Bwana wenu katika mbingu.


Maonyo

2 Mudumu katika kuomba. Munapoomba mukeshe na kumutolea Mungu shukrani.

3 Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.

4 Basi muniombee kusudi nipate kuupasha waziwazi sawa ninavyopaswa kufanya.

5 Mukuwe na mwenendo wa hekima mbele ya watu wanaokuwa wa inje ya kanisa, mukitumia vema kila wakati munaoupata.

6 Masemi yenu yanapaswa kuwa mazuri siku zote na yenye kufaa, munapaswa kujua kujibia kila mutu vizuri.


Salamu za mwisho

7 Ndugu yetu mupendwa Tikiko mutumishi mwaminifu, na mwenzangu tunayetumika naye kazi ya Bwana atawapasha ninyi habari zangu zote.

8 Ni kwa shabaha hiyo ninamutuma kwenu apate kuwajulisha habari zetu na kuwafariji.

9 Ninamutuma pamoja na ndugu mupendwa na mwaminifu, Onesimo, anayekuwa mwanainchi wa kule kwenu. Wao ndio watawaelezea maneno yote yaliyotokea hapa.

10 Mufungwa mwenzangu Aristarko anawasalimia. Naye Marko, binamu wa Barnaba anawasalimia vilevile. (Mumekwisha kupata maagizo juu ya Marko; akifika kwenu mumupokee vizuri).

11 Naye Yesu anayeitwa Yusto, anawasalimia ninyi vilevile. Kati ya Wayuda walioamini ni hao watatu tu ndio wanaotumika pamoja nami kwa ajili ya kazi inayoelekea Ufalme wa Mungu, nao wamenifariji sana.

12 Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.

13 Ninaweza kushuhudia juu yake kwamba anajisumbua sana kwa ajili yenu na kwa ajili ya wandugu wa Laodikia na wa Hierapoli.

14 Luka, muganga wetu mupendwa na Dema wanawasalimia.

15 Muwasalimie wandugu wa Laodikia, pamoja na Nimfa na kanisa linalokusanyika ndani ya nyumba yake.

16 Barua hii itakapokwisha kusomwa kwenu mufanye namna yote ipate kusomwa vilevile katika kanisa la Laodikia. Na ninyi kwa ngambo yenu, musome vilevile barua niliyotuma kwa kanisa lile.

17 Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.

18 Mimi Paulo ninawatumia salamu zangu, nikiziandika kwa mukono wangu mwenyewe. Musisahau kwamba mimi ningali katika kifungo. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan