Waefeso 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kazi ya Paulo kwa watu wa mataifa mengine 1 Kufuatana na mambo hayo, mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi watu wa mataifa mengine, ninamwomba Mungu. 2 Hakika, mumesikia jinsi Mungu alivyonijalia neema, akinipatia kazi ya kufanya kwa ajili yenu. 3 Mungu amenijulisha kwa njia ya ufunuo mupango wake uliofichwa. (Nimekwisha kuwaandikia kwa kifupi juu ya maneno haya. 4 Nanyi mukiyasoma mutaweza kutambua jinsi ninavyoelewa ule mupango wa Kristo uliofichwa.) 5 Zamani, Mungu hakuwajulisha watu mupango ule sawa vile ameujulisha sasa kwa mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho wake. 6 Nao mupango ule ni kwamba kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapewa sehemu yao ya urizi kutoka kwa Mungu pamoja na Wayuda. Watu wale ni viungo vya mwili mumoja, nao wanapokea vilevile sehemu ya vitu Mungu alivyoahidi kwa njia ya Yesu Kristo. 7 Nimewekwa kuwa mutumishi wa Habari Njema kwa njia ya zawadi Mungu aliyonipatia kutokana na uwezo wake. 8 Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa. 9 Na hivi nipate kuwaelezea vema namna unavyotimia ule mupango uliokuwa umefichwa tangu zamani na Mungu, muumbaji wa vitu vyote. 10 Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi. 11 Mungu amefanya hivi kufuatana na kusudi lake la milele alilofanya kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu. 12 Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa. 13 Basi ninawaomba musiregee kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, kwa maana yanawaletea utukufu. Ukubwa wa upendo wa Kristo 14 Kwa sababu hiyo ninapiga magoti mbele ya Baba Mungu, 15 anayekuwa asili ya jamaa zote zinazokuwa mbinguni na katika dunia. 16 Ninaomba Mungu, kwa uwingi wa utukufu wake, awajalie nguvu mupate kuwa imara ndani ya roho zenu, kwa njia ya Roho wake. 17 Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo. 18 Kwa hiyo ninyi pamoja na watu wote wa Mungu mutaweza kutambua katika ngambo zote ukubwa wa upendo wa Kristo unaopita kipimo. 19 Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa. 20 Basi, Mungu ambaye kwa nguvu yake inayofanya kazi ndani yetu, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi yanayopita yale tunayoweza kuomba au kufikiri; 21 atukuzwe katika kanisa na katika Yesu Kristo, kwa vizazi vyote kwa milele na milele. Amina. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo