Waebrania 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu Baba yetu 1 Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa. 2 Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu. 3 Kwa hiyo mumukumbuke yule aliyevumilia kutendewa na wenye zambi kwa chuki kubwa, kusudi musipate kuchoka wala kuregea. 4 Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa. 5 Na zaidi ya hii, mumesahau maonyo haya Mungu anayotoa kwenu kama wana wake? “Mwana wangu, usizarau azabu ya Bwana wala usiregee wakati anapokukaripia. 6 Kwa maana, Bwana anamwazibu yule anayemupenda, yeye anamupiga kila mutu anayemukubali kuwa mutu wake.” 7 Muvumilie maadibisho; kwa maana Mungu anawatendea ninyi kama wana wake. Tena, ni mwana gani asiyeazibiwa na baba yake? 8 Ikiwa hamuadibishwi na Mungu sawa vile watoto wake wote wanavyoadibishwa, basi ninyi si wana wa kweli wa Mungu, ninyi ni wana haramu. 9 Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi? 10 Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake. 11 Maadibisho yoyote wakati yanapotolewa yanaonekana kama ni tendo la huzuni wala si la furaha. Lakini kwa mwisho yanawaletea wale waliofundishwa nayo, maisha ya amani na ya haki. Maagizo na maonyo 12 Basi muitie tena nguvu mikono yenu inayopooza, nayo magoti yenu yanayoregea. 13 Mujitengenezee njia zenye kunyooka, kusudi mwenye ulema wa miguu asiteguke, lakini apate kupona. 14 Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana. 15 Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi. 16 Vilevile muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asikuwe mwasherati au mwenye kukufuru Mungu kama vile Esau aliyeuzisha haki yake ya muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kidogo tu. 17 Kama munavyojua, nyuma ya pale alikataliwa wakati alipotaka kupokea baraka toka kwa baba yake. Yeye hakukuwa tena na namna ya kugeuza tendo lake ijapokuwa alitafuta baraka ile kwa machozi. 18 Ninyi hamujafikia kwenye kitu kinachoweza kuguswa kama vile Waisraeli walivyofikia kwenye mulima Sinai. Mulima ule uliwaka moto, ulifunikwa na giza nzito, nao ulikuwa na uvumi wa zoruba juu yake. 19 Vilevile juu yake kulisikilika mulio wa baragumu na ngurumo ya sauti. Nao Waisraeli waliposikia sauti ile wakasihi wasiambiwe tena neno, 20 kwa sababu hawakuweza kuvumilia agizo walilotolewa: “Hata nyama akigusa mulima anapaswa kuuawa kwa kutupiwa mawe.” 21 Na mambo yale yaliyoonekana yalikuwa ya kuogopesha sana, hata Musa akasema: “Ninaogopa na kutetemeka!” 22 Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika. 23 Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu. 24 Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli. 25 Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni? 26 Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.” 27 Neno hili “mara moja tena” linaonyesha kwamba vitu vilivyoumbwa vitatikiswa na kutoweka, kusudi vile visivyoweza kutikiswa vipate kudumu. 28 Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga, 29 kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo