Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Waebrania 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu anasema na watu kwa njia ya Mwana wake

1 Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.

2 Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.

3 Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Kristo ni mukubwa kuliko wamalaika

4 Mwana amepata kuwa mukubwa kupita wamalaika kufuatana na lile jina alilopewa na Mungu, linalokuwa tukufu kuliko jina lao.

5 Kwa maana Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.” Wala hakusema maneno haya juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwana wangu.”

6 Na tena wakati Mungu alipomutuma muzaliwa wake wa kwanza katika dunia, alisema: “Wamalaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”

7 Lakini juu ya wamalaika, Mungu alisema: “Mungu anawafanya wamalaika wake kuwa kama upepo. Anawafanya hao watumishi wake kuwa kama ndimi za moto.”

8 Lakini juu ya Mwana, Mungu alisema: “Kiti chako cha kifalme, Ee Mungu, kitadumu hata milele. Unatawala ufalme wako kwa haki.

9 Unapenda haki na kuchukia uovu. Ni kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekusimika, akikupakaa mafuta, akikupatia heshima na kukuinua juu kuliko wenzako wote.”

10 Vilevile Mungu alisema: “Wewe Bwana, kwa mwanzo uliumba dunia, mbingu ni kazi ya mikono yako.

11 Vitatoweka lakini wewe utabaki. Vitachakaa kama nguo.

12 Utavikunjakunja kama kanzu, navyo vitabadilishwa kama nguo. Lakini wewe utabaki sawasawa, na maisha yako hayatakuwa na mwisho.”

13 Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu, mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”

14 Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan