Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Ufunuo 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha malaika wa tano akapiga baragumu. Halafu nikaona nyota iliyokuwa imeshuka toka mbinguni, na kuanguka katika dunia. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo ndefu la kuzimu.

2 Nyota ile ikafungua hilo shimo. Moshi unaokuwa kama moshi wa furu kubwa ukapanda toka ndani ya shimo lile. Giza la ule moshi uliotoka ndani ya lile shimo ulifunika jua na anga.

3 Nzige wakatokea katika ule moshi, na kusambaa juu ya dunia. Nao wakapewa nguvu zinazokuwa kama za nge.

4 Wakaambiwa wasiharibu majani yoyote wala mumea wowote, wala muti wowote, lakini wawatese watu wasiokuwa na chapa ya muhuri wa Mungu kwenye paji za nyuso zao.

5 Nzige wale hawakupewa amri ya kuwaua watu wale, lakini wawatese kwa muda wa miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama vile nge wakati anapouma mutu.

6 Na kwa muda ule, watu watatafuta kifo, lakini hakitawapata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.

7 Umbo la nzige wale lilifanana na farasi waliopambwa kwa kupigana vita. Juu ya vichwa vyao kulikuwa vitu vinavyofanana na taji za zahabu, na nyuso zao zilifanana kama nyuso za watu.

8 Nywele zao zilikuwa sawa nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.

9 Na juu ya vifua vyao kulikuwa vitu vinavyofanana na ngao za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama uvumi wa magari yanayovutwa na farasi wengi wanaokimbia mbio kwenda kwa vita.

10 Walikuwa na mikia kama ya nge na yenye kuchoma kama miiba. Uwezo wao wa kuwatesa watu kwa muda wa ile miezi mitano ulikuwa ndani ya mikia yao.

11 Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).

12 Hasara ya kwanza imepita, na nyuma ya ile kutatokea hasara zingine mbili.

13 Malaika wa sita akapiga baragumu. Halafu nikasikia sauti moja ikitokea kwenye pembe ine za mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.

14 Sauti ile ikamwambia yule malaika wa sita aliyeshika baragumu hivi: “Uwafungue wale wamalaika wane waliofungwa kwenye muto mukubwa Furati.”

15 Wale wamalaika wane wakafunguliwa, nao walikuwa wamewekwa tayari kwa saa ile, siku, mwezi na mwaka ule, wapate kuua sehemu moja ya tatu ya wanadamu.

16 Nikasikia hesabu ya makundi ya waaskari wapanda-farasi, nao walikuwa milioni mia mbili.

17 Na katika maono yale, nikaona wale farasi pamoja na wale waaskari waliopanda juu yao. Waaskari wale walikuwa na ngao zenye rangi nyekundu kama moto na zingine za rangi ya samawi na ya kimanjano kama kiberiti. Vichwa vya farasi wale vilikuwa kama vichwa vya simba, na ndani ya vinywa vyao mulitoka moto, moshi na mawe ya viberiti.

18 Na sehemu moja ya tatu ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu: kwa moto, moshi na viberiti vilivyotoka ndani ya vinywa vya wale farasi,

19 kwa maana uwezo wa wale farasi ulikuwa ndani ya vinywa vyao na ya mikia yao vilevile. Mikia yao ilikuwa kama kichwa cha nyoka, na kwa mikia hiyo waliweza kuzuru watu.

20 Watu waliobaki bila kuuawa na yale mapigo hawakuachana na sanamu walizojitengenezea wao wenyewe. Hawakuacha kuabudu pepo, sanamu za zahabu, za feza, za shaba, za mawe na za miti zisizoweza kuona, wala kusikia, wala kutembea.

21 Watu wale hawakuacha hata matendo yao ya uuaji, ya uchawi, ya uasherati na ya wizi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan