Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Ufunuo 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kizingo cha karatasi na Mwana-Kondoo

1 Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.

2 Nikaona malaika mwenye uwezo aliyekuwa akitangaza hivi kwa sauti kubwa: “Ni nani anayestahili kuvunja vile vifundo vya mihuri na kufungua kizingo kile?”

3 Lakini hakukuwa hata mutu mbinguni, wala katika dunia, wala katika kuzimu aliyeweza kufungua kizingo kile na kuangalia ndani yake.

4 Nami nikalia sana, kwa sababu hakukuonekana mutu aliyestahili kufungua kizingo wala kuangalia ndani yake.

5 Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”

6 Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.

7 Yule Mwana-Kondoo akajongea na kukamata kizingo kutoka mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme.

8 Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.

9 Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.

10 Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”

11 Kisha nikaangalia tena, nikasikia sauti ya wamalaika wengi wenye kuzunguka kiti cha kifalme, na viumbe vya ajabu na wazee. Hesabu yao ilikuwa maelfu na maelfu na mamilioni na mamilioni.

12 Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”

13 Nikasikia vilevile viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni, katika dunia, katika kuzimu na vile vinavyokuwa katika bahari; viumbe vyote vya ulimwengu nzima vikimwimbia: “Utukufu, heshima, sifa na nguvu milele na milele, kwa yule anayeikaa juu kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo.”

14 Vile viumbe vine vya ajabu vilijibu: “Amina.” Na wale wazee wakainama uso mpaka chini na kuabudu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan