Ufunuo 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Ujumbe kwa kanisa la Sardi 1 “Umwandikie malaika wa kanisa la Sardi hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa na roho zile saba za Mungu na zile nyota saba. Ninajua matendo yako, hakika wewe umekwisha kufa ingawa unajulikana kuwa muzima. 2 Amuka! Uimarishe kile kinachobaki kinachokaribia kufa, kwa maana nimeona kwamba matendo yako si makamilifu mbele ya Mungu wangu. 3 Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako. 4 Lakini ungali na watu wachache kule Sardi wasiochafua nguo zao. Wale ndio watakaotembea pamoja nami wakivaa nguo nyeupe kwa sababu wanastahili. 5 Yule atakayeshinda atavalishwa nguo nyeupe, nami sitafuta jina lake kati ya majina yanayoandikwa katika kitabu cha uzima. Nami nitamutetea mbele ya Baba yangu na mbele ya wamalaika zake. 6 “Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! Ujumbe kwa kanisa la Filadelfia 7 “Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua. 8 Ninajua matendo yako. Ninajua kwamba wewe hauna uwezo mwingi, lakini umeshika neno langu, nawe haukukana jina langu. Basi nimefungua mulango wazi mbele yako, wala hakuna anayeweza kuufunga. 9 Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda. 10 Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake. 11 Ninakuja upesi. Shika sana kile unachokuwa nacho, kusudi mutu yeyote asinyanganye taji yako ya ushindi. 12 Yule atakayeshinda nitamufanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hatatoka tena mule. Na zaidi ya ile nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la muji wa Mungu wangu, ndio Yerusalema mupya, utakaoshuka toka mbinguni kwa Mungu wangu. Nitaandika vilevile juu yake jina langu jipya. 13 “Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa. Ujumbe kwa kanisa la Laodikia 14 “Umwandikie malaika wa kanisa la Laodikia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeitwa ‘Amina’, mushuhuda mwaminifu, mwenye ukweli, na musingi wa viumbe vyote vya Mungu. 15 Ninajua matendo yako: wewe si baridi wala si moto. Afazali ungekuwa baridi tu au moto tu. 16 Lakini sasa kwa sababu wewe ni mwenye uvuguvugu, ni kusema hauko baridi wala moto, nitakutapika kutoka katika kinywa changu. 17 Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi. 18 Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona. 19 Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi. 20 Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami. 21 Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme. 22 “Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo