Ufunuo 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mbingu mupya na dunia mupya 1 Kisha nikaona mbingu mupya na dunia mupya. Kwa sababu mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimekwisha kutoweka, bahari nayo haikukuwa tena. 2 Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake. 3 Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao. 4 Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.” 5 Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.” 6 Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa. 7 Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu. 8 Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.” Yerusalema mupya 9 Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.” 10 Nikashikwa na Roho, na malaika akanipeleka juu ya mulima mukubwa na murefu. Akanionyesha muji mutakatifu, ndio Yerusalema uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, 11 nao ukingaa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la bei kali la yaspi, linalongaa kama kioo. 12 Ulikuwa ukizungukwa na ukuta mukubwa na murefu wenye milango kumi na miwili na wamalaika kumi na wawili walichunga milango ile. Na juu ya milango ile, kulikuwa kumeandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya Waisraeli. 13 Kila upande kulikuwa milango mitatu: upande wa mashariki milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, upande kusini milango mitatu na upande wa magaribi milango mitatu. 14 Na ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa umejengwa juu ya mawe ya musingi kumi na mawili na juu ya kila jiwe kulikuwa kumeandikwa jina la kila mumoja wa mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo. 15 Malaika yule aliyekuwa akisema nami alikuwa na fimbo ya kupima ya zahabu kusudi apate kupima muji ule, milango yake na ukuta unaouzunguka. 16 Muji ule ulikuwa umejengwa namna ya muraba, urefu wake na upana wake vilikuwa sawasawa. Malaika akapima muji ule na ile fimbo; ulikuwa na urefu, upana na urefu wake wa kwenda juu yapata kilometre elfu mbili na mia ine. 17 Malaika akapima vilevile ukuta; ulikuwa yapata metre makumi sita kufuatana na kipimo cha kawaida cha wanadamu ambacho yule malaika alichotumia. 18 Ukuta ulikuwa umejengwa na mawe ya bei kali ya yaspi, na muji wenyewe ulikuwa umejengwa na zahabu safi inayongaa kama kioo. 19 Musingi wa ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa unapambwa na mawe ya bei kali ya kila aina. Mawe ya musingi wa kwanza ulikuwa wa mawe ya yaspi, wa pili wa mawe ya safilo, wa tatu wa mawe ya kaledoni, wa ine wa mawe ya zumaridi, 20 wa tano wa mawe ya sadoniki, wa sita wa mawe ya akiki, wa saba wa mawe ya krisolite, wa nane wa mawe ya belulo, wa tisa wa mawe ya topazo, wa kumi wa mawe ya krisoparazo, wa kumi na moja wa mawe ya haikinto na wa kumi na mbili wa mawe ya amazito. 21 Na ile milango kumi na miwili ilikuwa ushanga nzuri kumi na mbili; kila mulango ulikuwa umetengenezwa na ushanga moja. Barabara ya muji ule ilikuwa imetengenezwa na zahabu safi inayongaa kama kioo. 22 Sikuona hekalu ndani ya muji ule, maana Bwana wetu Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwana-Kondoo ndio hekalu lake. 23 Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. 24 Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake. 25 Milango ya muji ule haitafungwa muchana maana ndani yake hakutakuwa usiku. 26 Heshima na utukufu za watu wote wa mataifa zitaletwa ndani ya muji ule. 27 Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo