Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Tito 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mafundisho ya kweli

1 Lakini kwa ngambo yako, ufundishe maneno yale yanayolingana na mafundisho ya kweli.

2 Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.

3 Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.

4 Kwa njia hii wataweza kuwafundisha vijana wanawake kuwapenda waume wao na watoto wao,

5 na kuwa wenye utaratibu, wenye maisha safi, wenye kutunza nyumba zao vizuri, wema na wenye kutii waume wao, kusudi Neno la Mungu lisitukaniwe.

6 Vilevile uwaonye vijana wanaume wakuwe wenye utaratibu katika mambo yote.

7 Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.

8 Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.

9 Sherti watumwa watii wabwana wao katika mambo yote na kuwapendeza, wakiepuka kubishana nao

10 na kuiba vitu vyao. Lakini wajionyeshe kila mara kuwa waaminifu kamili, kusudi wapate kuheshimisha mafundisho juu ya Mungu Mwokozi wetu katika mambo yote.

11 Kwa maana neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote imeonekana waziwazi.

12 Neema hii inatufundisha kwamba tuache uovu na tamaa za dunia, na kuishi katika dunia hii ya sasa katika ukadirifu, katika haki na kushikamana na ibada.

13 Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.

14 Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.

15 Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan