Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Obadia 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!


Yawe ataazibu taifa la Edomu

2 Yawe aliambia taifa la Edomu: Nitakufanya kuwa mudogo kati ya mataifa, utazarauliwa kabisa na wote.

3 Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?

4 Hata ukiruka juu kama tai, ukifanya makao yako kati ya nyota, mimi nitakushusha chini tu. –Ni ujumbe wa Yawe.

5 Kama wizi au wanyanganyi wangekufikia usiku, si wao wangekuiba tu vitu wanavyokuwa navyo lazima? Ikiwa wavunaji wa zabibu wangekufikia, si wangekuachia sehemu ndogo tu? Lakini wewe, waadui zako wamekuangamiza kabisa.

6 Enyi wazao wa Esau, mali yenu imenyanganywa, akiba zenu zote zilizofichwa zimevumbuliwa!

7 Washirika wenzenu wamewadanganya, wamewafukuza toka katika inchi yenu. Watu muliopatana nao wamewashinda katika vita. Warafiki wa kutegemewa ndio waliokutegea mitego, nawe haukuelewa yaliyokuwa yanatendeka.

8 Mimi Yawe ninakuuliza hivi: Siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mulima wa wazao wa Esau?

9 Ewe muji wa Temani, mashujaa wako wataogopa na kila mutu juu ya mulima wa wazao wa Esau.


Sababu za kuazibiwa kwa taifa la Edomu

10 Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.

11 Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu, wakati wageni walipouteka utajiri wao, walipoingia katika milango yake na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura. Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.

12 Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,

13 hamukupaswa kuingia katika muji wa watu wangu, siku walipopatwa na hasara, hamukupaswa kukamata mali zao, siku hiyo ya hasara yao,

14 hamukupaswa kusimama kwenye masanganjia na kuwakamata wakimbizi wao, hamukupaswa kuwatoa kwa waadui zao wale waliobaki wazima.


Mungu atayahukumu mataifa

15 Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.

16 Maana, kama walivyokunywa kikombe cha kasirani yangu kwenye mulima wangu mutakatifu, ndivyo mataifa jirani watakavyokunywa; watakunywa na kupepesuka, wataangamia na kuwa kama hawakukuwa mbele katika dunia.


Waisraeli watashinda

17 Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni nao utakuwa mulima mutakatifu. Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.

18 Wazao wa Yakobo watakuwa kama moto na wazao wa Yosefu kama ndimi za moto. Watawaangamiza wazao wa Esau kama vile moto unavyoteketeza majani yenye kukauka, hakutaponyoka hata mumoja wao. –Yawe amesema.

19 Wale wanaokaa Negebu wataurizi mulima wa wazao wa Esau, wale wanaokaa katika Shefela watarizi inchi ya Wafilistini. Waisraeli watarizi inchi za Efuraimu na Samaria na watu wa kabila la Benjamina watarizi inchi ya Gileadi.

20 Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho, lile jeshi la Waisraeli, watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata. Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi watarizi miji ya Negebu.

21 Wakombozi watapanda juu ya mulima Sayuni kwa kuutawala mulima wa wazao wa Esau; naye Yawe atakuwa ndiye Mufalme.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan