Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Nehemia 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Wamasikini wanateswa

1 Nyuma ya muda kukatokea malalamiko kati ya watu, wanaume na wanawake, wakiwalalamikia wandugu zao Wayuda.

2 Kukatokea waliosema: “Tafazali mutupatie ngano tukule kusudi tuweze kuishi kwa sababu sisi, wana wetu na wabinti zetu tuko wengi.”

3 Na wengine wakalalamika: “Tumeweka rehani mashamba yetu, mizabibu yetu hata na nyumba zetu kwa kupata ngano kwa sababu ya njaa.”

4 Tena kukakuwa hata wale, waliolalamika, wakisema: “Kwa kulipa kodi ya mufalme juu ya mashamba na mizabibu yetu, tulipaswa kukopesha feza.

5 Lakini sisi ni sawa na Wayuda wengine; watoto wetu ni sawa na watoto wao. Hata hivyo, tunawalazimisha watoto wetu kuwa watumwa. Wabinti zetu wamoja wamekwisha kuwa watumwa. Hatuna uwezo wa kuzuia jambo hili maana mashamba yetu na mizabibu yetu inanyanganywa na watu wengine.”

6 Niliposikia malalamiko yao, nikakasirika sana.

7 Nikaamua kukamata hatua. Nikawaonya wakubwa na wasimamizi, nikawaambia: “Munawatesa wandugu zenu.”

8 Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.

9 Kisha nikawaambia: “Jambo munalofanya si zuri. Haiwapasi kumwogopa Mungu wetu kwa kuzuia mataifa mengine yanayokuwa waadui zetu yasituzarau?

10 Zaidi ya hayo, mimi mwenyewe, wandugu zangu na watumishi wangu tumewakopesha wandugu zetu feza na ngano. Na hatutadai faida yoyote.

11 Leo hii muwarudishie mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na nyumba zao, hata na faida ya feza, ngano, divai, na mafuta ambayo mulikuwa munawalipisha.”

12 Wao wakaitikia na kusema: “Tutawarudishia na hatutawadai chochote. Tutafanya kama vile ulivyosema.” Nikawaita makuhani mbele, na viongozi wote wakaapa mbele ya makuhani kufanya kama walivyoahidi.

13 Nikakunguta upindo wa kanzu yangu na kusema: “Kila mumoja asiyetimiza ahadi hii Mungu amukungute, amutoe katika nyumba yake na katika kazi yake. Basi, akungutike na kubaki mikono mitupu.” Mukutano muzima wakaitikia, na kusema: “Amina”; wakamusifu Yawe. Watu wakafanya kama vile walivyokuwa wameahidi.


Tabia ya Nehemia

14 Tangu wakati nilipochaguliwa kuwa mutawala wa inchi ya Yuda kwa miaka kumi na miwili ni kusema tangu mwaka wa makumi mbili mpaka mwaka wa makumi tatu na mbili wa utawala kwa mufalme Artasasta, sikukula chakula kinachostahili kukuliwa na mutawala, wala wandugu zangu hawakufanya hivyo.

15 Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.

16 Nilikuwa na juhudi nyingi katika ujenzi mupya wa ukuta huu na sikujipatia hata shamba. Hata watumishi wangu wote walifanya kazi hii kwa bidii.

17 Zaidi ya hayo, kila siku niliwakulisha watu mia moja na makumi tano, kati yao kukiwa Wayuda na wakubwa zaidi ya wale watu waliotufikia toka mataifa jirani.

18 Kila siku, kwa kuwalisha watu hao, nilichinjiwa ngombe dume mumoja na kondoo safi sita na kuku. Kila mara kisha siku kumi nilitoa divai kwa wingi. Lakini zaidi ya haya yote, kwa sababu watu walikuwa na muzigo muzito wa kubeba kila siku, sikutaka posho ya zaidi.

19 Sasa, Ee Mungu wangu, kumbuka wema wangu wote niliowatendea watu hawa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan