Nehemia 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Watu waliokaa Yerusalema 1 Kisha, viongozi wa watu wakakaa katika Yerusalema; watu wengine wote, wakapiga kura kati ya kila jamaa kumi kwa kuchagua jamaa moja itakayokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu. Jamaa zingine tisa zikakaa katika miji yao mingine. 2 Watu wakawasifu wale wote waliokubali kukaa katika Yerusalema. 3 Na katika miji mingine, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango na wazao wa watumishi wa Solomono, walikaa katika maeneo yao wenyewe, katika miji yao. 4 Watu wamoja wa kabila la Yuda na wa kabila la Benjamina walikaa katika Yerusalema: Hawa ndio watu wa ukoo wa Yuda waliokaa Yerusalema: Ataya mwana wa Uzia, mujukuu wa Zakaria mwana wa Amaria mwana wa Sefatia mwana wa Mahalaleli wa uzao wa Peresi; 5 Maseya mwana wa Baruku mwana wa Koli-Hoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria, Mushilo. 6 Wazao wote wa Peresi waliokaa katika Yerusalema walikuwa wanaume mashujaa mia ine makumi sita na wanane. 7 Watu wa ukoo wa Benjamina waliokaa katika Yerusalema ni: Salu, mwana wa Mesulamu mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maseya mwana wa Itieli na mwana wa Yesaya. 8 Nyuma ya huyo kulikuwa Gabayi na Salayi. Jumla yao mia tisa makumi mbili na wanane. 9 Yoeli mwana wa Sikiri, alikuwa ndiye mukubwa wao; naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa mukubwa wa pili wa muji. 10 Makuhani waliokaa katika Yerusalema walikuwa: Yedaya mwana wa Yoyaribu, Yakini, 11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Mesulamu mwana wa Zadoki mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya Mungu, 12 pamoja na wandugu zao waliofanya kazi katika hekalu walikuwa mia nane makumi mbili na wawili. Pamoja na hao, kulikuwa Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia mwana wa Amsi mwana wa Zakaria mwana wa Pasuri mwana wa Malkiya; 13 vilevile wandugu zake waliokuwa wakubwa wa jamaa za baba zao; wote pamoja walikuwa watu mia mbili makumi ine na wawili. Vilevile kulikuwa Amasayi, mwana wa Azareli mwana wa Azayi mwana wa Mesilemoti mwana wa Imeri, 14 pamoja na wandugu zao; wote wakiwa mia moja makumi mbili na wanane, watu mashujaa. Na mukubwa wao alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu. 15 Nao Walawi waliokaa katika Yerusalema walikuwa: Semaya mwana wa Hasubu mwana wa Azirikamu mwana wa Hasabia, na mwana wa Buni. 16 Sabetayi na Yozabadi, wakubwa wa ukoo wa Walawi, walikuwa wasimamizi wa kazi za inje ya nyumba ya Mungu, 17 na Matania mwana wa Mika mwana wa Zabudi, wa uzao wa Asafu, aliyekuwa kiongozi wakati wa kuomba maombi ya shukrani. Bakubukia alikuwa musaidizi wake. Pamoja nao kulikuwa Abuda mwana wa Samua mwana wa Galali wa uzao wa Yedutuni. 18 Walawi wote waliokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu, walikuwa mia mbili makumi munane na wane. 19 Walinzi wa milango waliokaa katika Yerusalema walikuwa: Akubu na Talmoni pamoja na wandugu zao waliokuwa wakilinda milango, walikuwa mia moja makumi saba na wawili. 20 Watu wengine wa Israeli, makuhani na Walawi walikaa katika miji ya Yuda, kila mumoja katika urizi wake. 21 Lakini watumishi wa hekalu walikaa Yerusalema katika eneo la Ofeli wakiwa chini ya usimamizi wa Ziha na Gisipa. 22 Kiongozi wa Walawi waliokaa Yerusalema alikuwa, Uzi, mwana wa Bani mwana wa Hasabia mwana wa Matania mwana wa Mika wa ukoo wa Asafu, waliokuwa waimbaji, viongozi waangalizi wa shuguli za nyumba ya Mungu. 23 Mufalme alikuwa ametoa amri juu ya utaratibu wa kazi zao na mahitaji yao ya kila siku. 24 Petahia mwana wa Mesezabeli, wa ukoo wa Zera katika kabila la Yuda, alikuwa musimamizi wa mufalme juu ya mambo yote ya watu wa Yuda. Watu wa miji mingine 25 Watu wengine walikaa katika miji karibu na mashamba yao. Watu wamoja wa kabila la Yuda walikaa Kiriati-Arba, Diboni na Yekabuseli pamoja na vijiji vilivyoizunguka. 26 Wengine vilevile walikaa katika miji ya Yesua, Molada, Beti-Peleti, 27 Hazari-Suali na Beri-Seba pamoja na vijiji vilivyoizunguka. 28 Wengine walikaa katika muji wa Ziklagi, Mekona na vijiji vilivyoizunguka. 29 Wengine walikaa katika miji ya Eni-Rimoni, Sora, Yarmuti; 30 Zanoa na Adulamu pamoja na vijiji vilivyoizunguka, Lakisi na mashamba yanayouzunguka, na katika Azeka pamoja na vijiji vinavyouzunguka. Hii ina maana kwamba watu wa Yuda walikaa katika eneo linalokuwa kati ya Beri-Seba upande wa kusini na Bonde la Hinomu upande wa Kaskazini. 31 Watu wa kabila la Benjamina walikaa Geba, Mikimasi, Ai, Beteli na vijiji vinavyoizunguka. 32 Wengine walikaa Anatoti, Nobu, Anania, 33 Hazori, Rama, Gitaimu, 34 Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35 Lodi na Ono lililokuwa Bonde la Wafundi. 36 Walawi wamoja wa Yuda wakachanganyika na watu wa Benjamina. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo