Nehemia 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Watu wanatia sahihi juu ya mapatano 1 Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara kwa maandiko na wakubwa wetu, Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na muhuri wao. 2-9 Haya ndiyo majina yao: Liwali wa jimbo: Nehemia, mwana wa Hakalia. Makuhani: Zedekia, Seraya, Azaria, Yeremia, Pasuri, Amaria, Malkiya, Hatusi, Sebania, Maluku, Harimu, Meremoti, Obadia, Danieli, Ginetoni, Baruku, Mesulamu, Abiya, Miyamini, Masia, Bilgayi, Semaya. 10-14 Walawi: Yesua mwana wa Azania, Binui wa uzao wa Henadadi, Kadimieli na wandugu zao: Sebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani, Mika, Rehobu, Hasabia, Zakuri, Serebia, Sebania, Hodia, Bani, Beninu. 15-28 Viongozi wa watu: Parosi, Pahati-Moabu, Elamu, Zatu, Bani, Buni, Azgadi, Bebayi, Adonia, Bigwayi, Adini, Ateri, Hezekia, Azuri, Hodia, Hashumu, Bezayi, Harifu, Anatoti, Nobayi, Magipiasi, Mesulamu, Hesiri, Mesezabeli, Zadoki, Yadua, Pelatia, Hanani, Anaya, Hosea, Hanania, Hasubu, Halohesi, Pileha, Sobeki, Rehumu, Hasabuna, Maseya, Ahia, Hanani, Anani, Maluku, Harimu na Bana. Ahadi 29 Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu, 30 tunaungana na wandugu zetu, wakubwa wetu, katika kufanya kiapo na kwamba tukivunja kiapo hiki tutapata azabu, na tunaapa kwamba tutaishi kwa kufuata sheria ya Mungu ambayo alitoa kwa njia ya Musa, mutumishi wake; tena tutatii yote ambayo Yawe, Mungu wetu, anatuamuru; na kwamba tutashika maagizo na masharti yake. 31 Wabinti zetu hatutawaoesha kwa watu wa inchi hii na wala wana wetu hawataoa kwao. 32 Ikiwa watu hao wanaleta biashara au ngano kwa kuuzisha siku ya Sabato, sisi hatutanunua siku hiyo wala siku nyingine yoyote inayokuwa takatifu. Mwaka wa saba hatutalima mashamba na madeni yote tutayafuta. 33 Tunajiwekea sheria juu yetu kwamba, kwa mwaka tutatoa sehemu moja ya tatu ya kikoroti kimoja cha feza kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu: 34 kwa ajili ya mikate mitakatifu, sadaka za unga za kawaida, sadaka za kuteketezwa kwa moto za kawaida, sadaka za siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, sikukuu nyingine zilizowekwa, vitu vingine vitakatifu, sadaka za kusamehewa zambi, kwa kuwafanyia upatanisho watu wa Israeli na kazi nyingine zozote za nyumba ya Mungu wetu. 35 Sisi wote, watu wote, makuhani na Walawi tutapiga kura kila mwaka kwa kuchagua ukoo utakaoleta kuni za kuteketeza sadaka juu ya mazabahu ya Yawe, Mungu wetu, kufuatana na Sheria. 36 Tunaahidi kuleta kila mwaka malimbuko yetu ya mazao na ya matunda ya kila muti kwenye nyumba ya Yawe. 37 Kwa kufuata vile ilivyoandikwa katika Sheria kila muzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wana wetu, katika nyumba zetu, atapelekwa katika nyumba ya Mungu wetu kwa makuhani wanaotumika mule, vilevile tutapeleka kila muzaliwa wa kwanza dume wa ngombe zetu, mbuzi zetu na kondoo zetu. 38 Kila unga wetu wa kwanza, matoleo yetu, matunda ya miti, divai na mafuta tutavileta kwa kuhani kwenye vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Tena tutaleta zaka zetu za mazao yetu kwa Walawi, maana ndio wanaoshugulika na kukusanya zaka zile katika vijiji vyetu. 39 Kuhani, wa uzao wa Haruni atakuwa pamoja na Walawi wanapokea zaka. Halafu Walawi watapeleka sehemu moja ya kumi ya zaka zote zilizotolewa katika nyumba ya Mungu kwenye vyumba na gala. 40 Watu wa Israeli na Walawi watayapeleka matoleo ya ngano, divai na mafuta ya zeituni kwenye vyumba ambamo vyombo vya Pahali Patakatifu vinapochungwa na ambamo makuhani, walinzi wa milango na waimbaji wana vyumba vyao. Na siku zote tutashugulikia nyumba ya Mungu wetu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo