Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mwanzo 43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Benjamina anakwenda Misri

1 Kisha njaa ikazidi kuwa kali katika inchi ya Kanana.

2 Kisha kumalizika kwa kile chakula walichokuwa wamenunua kutoka Misri, Yakobo akawaambia wana wake: “Mwende tena Misri, mutununulie chakula kidogo.”

3 Lakini Yuda akamwambia baba yake: “Yule mutu alituonya vikali, akisema: ‘Sitawapokea musipokuja na ndugu yenu mudogo.’

4 Kama utakubali ndugu yetu kwenda pamoja nasi, basi tutakwenda kukununua chakula.

5 Lakini ikiwa hautakubali aende nasi, basi, hatutakwenda kule, maana yule mutu alituambia waziwazi: ‘Hamutaniona musipokuja na ndugu yenu mudogo.’ ”

6 Israeli akasema: “Kwa nini mulinitia katika taabu kwa kumwambia yule mutu kwamba muko na ndugu mwingine?”

7 Wakamujibu: “Yule mutu alituuliza kwa makali sana juu ya mambo yetu na jamaa yetu akisema: ‘Baba yenu angali muzima? Muko na ndugu mwingine?’ Hivyo tukamujibu kulingana na maulizo yake. Tungaliweza namna gani kujua kwamba atatuambia: ‘Mulete ndugu yenu?’ ”

8 Yuda akamwambia baba yake Israeli: “Uniruhusu mimi niende naye kusudi tuondoke mara moja, tuende tununue chakula, tusikufe na njaa pamoja nawe na watoto wetu.

9 Mimi mwenyewe nitakuwa rehani kwake. Wewe utanidai mimi. Nisipomurudisha umwone kwa macho yako mwenyewe, kosa likuwe juu yangu milele.

10 Kama tusingalikawia, tungalikuwa tumekwisha kwenda na kurudi mara mbili.”

11 Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.

12 Mupeleke feza mara mbili ya ile inayohitajika, kwa sababu ni lazima murudishe feza ile iliyowekwa kwenye kinywa cha mifuko yenu; pengine ilirudishwa kwa makosa.

13 Mumupeleke vilevile ndugu yenu muende kwa yule mutu.

14 Mungu Mwenye Nguvu awajalie kupata huruma mbele ya mutu yule, awaachie yule ndugu yenu mwingine na Benjamina warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kupotelewa na wana wangu, basi!”

15 Basi, wakatwaa zile zawadi na feza mara mbili ya ile ya mbele, wakakwenda Misri pamoja na ndugu yao Benjamina. Walipofika, wakakwenda na kusimama mbele ya Yosefu.

16 Yosefu alipomwona Benjamina pamoja nao, akamwambia musimamizi wa nyumba yake: “Uwapeleke watu hawa kwenye nyumba, uchinje nyama mumoja na kumutengeneza vizuri, maana watu hawa watakula nami chakula cha muchana.”

17 Musimamizi yule akafanya kama vile alivyoagizwa. Akawapeleka wale wageni kwenye nyumba ya Yosefu.

18 Walipoona wamepelekwa kwenye nyumba ya Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao: “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile feza tuliyorudishiwa katika mifuko yetu tulipokuja safari ya kwanza kusudi apate kisingizio cha kutushambulia kwa rafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.”

19 Kwa hiyo wakamwendea yule musimamizi wa nyumba ya Yosefu wakaongea naye wakiwa kwa mulango,

20 wakamwambia: “Tafazali, bwana! Sisi tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula.

21 Tulipofika pahali pa kulala wageni kule katika njia, tukafungua mifuko yetu, tukashangaa kukuta feza ya kila mumoja wetu kwenye kinywa cha mufuko wake bila kuguswa. Sasa tumerudisha feza hiyo.

22 Tumeleta na feza ingine kwa kununua chakula. Hatujui ni nani aliyeweka feza yetu katika mifuko yetu.”

23 Yule musimamizi akawajibu: “Musikuwe na wasiwasi, wala musiogope. Bila shaka Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, ndiye aliyewarudishia feza katika mifuko yenu. Mimi nilipokea feza yenu.” Kisha akawaletea Simeoni, ndugu yao.

24 Yule musimamizi alipowakaribisha ndani ya nyumba kwa Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu yao, na punda wao akawakulisha.

25 Nao wakatayarisha zawadi zao za kumupa Yosefu, kwa sababu walisikia kwamba watakula pamoja naye.

26 Yosefu, aliporudi kwake, wakamuletea zile zawadi walizokuwa nazo, wakainama mbele yake kwa heshima.

27 Yosefu akawauliza habari zao na kusema: “Mulinielezea habari za muzee, baba yenu. Yuko salama? Angali muzima?”

28 Wakamujibu: “Mutumishi wako, baba yetu, yuko salama na angali muzima.” Kisha wakainama kwa heshima.

29 Yosefu alipoinua macho yake na kumwona Benjamina, ndugu yake, mutoto wa mama yake, akasema: “Huyu ndiye ndugu yenu mudogo muliyeniambia habari zake? Mungu akubariki, mwana wangu!”

30 Yosefu akatoka pahali pale kwa haraka, kwa sababu ya hamu kubwa juu ya ndugu yake, akatafuta pahali pa kulilia. Akaingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia.

31 Kisha kunawa uso wake, akatoka, akijikaza, akaamuru wamuletee chakula.

32 Yosefu alitayarishiwa chakula chake peke yake, na wandugu zake wakatayarishiwa peke yao. Vilevile Wamisri waliokula pamoja naye, wakatayarishiwa peke yao, maana ni chukizo kwa Wamisri kula chakula pamoja na Waebrania.

33 Wandugu za Yosefu waliikaa mbele yake kulingana na umri wao, kuanzia wa kwanza mpaka wa mwisho. Wakakuwa wanaangaliana kwa mushangao.

34 Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan