Mwanzo 37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Yosefu na wandugu zake Wafalme wa inchi ya Edomu ( 1 Sik 1.43-54 ) 1 Yakobo akaendelea kukaa katika inchi ya Kanana, ambamo baba yake aliishi kama mugeni. 2 Hizi ndizo habari za ukoo wa Yakobo. Yosefu, akiwa kijana wa umri wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo na mbuzi pamoja na wandugu zake, wana wa Biliha na Zilpa, wake za baba yake. Yosefu akakuwa anamujulisha baba yake juu ya tabia mbaya za wandugu zake. 3 Israeli alimupenda Yosefu kuliko watoto wake wote kwa sababu alikuwa amezaliwa wakati wa uzee wake. Alimupa Yosefu kanzu nzuri sana. 4 Lakini wandugu zake walipoona kwamba baba yao alimupenda Yosefu kuliko wao, wakamuchukia hata hawakuzungumuza naye kwa amani. Ndoto za Yosefu 5 Usiku mumoja, Yosefu akaota ndoto, lakini alipowaelezea wandugu zake, wao wakazidi kumuchukia. 6 Aliwaambia: “Musikilize ndoto niliyoota: 7 Niliota kwamba sisi wote tulikuwa katika shamba tukifunga miganda. Kwa rafla muganda wangu ukainuka na kusimama wima. Miganda yenu ikakusanyika kuuzunguka na kuinamia mbele ya muganda wangu.” 8 Wandugu zake wakamwuliza: “Unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumuchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake. 9 Kisha Yosefu akaota ndoto ingine, akawaelezea wandugu zake akisema: “Musikilize, nimeota ndoto nyingine. Nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinainamia mbele yangu.” 10 Lakini alipomwelezea baba yake na wandugu zake ndoto hiyo, baba yake alimukaripia, akisema: “Ni ndoto gani hiyo uliyoota? Itatupasa mimi, mama yako na wandugu zako kuja kuinama chini kwa heshima mbele yako?” 11 Wandugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akakuwa anafikiri juu ya jambo hilo. Yosefu anauzishwa 12 Siku moja, wandugu za Yosefu wakakwenda kuchunga nyama wa baba yao karibu na Sekemu. 13 Basi, Israeli akamwambia Yosefu: “Unajua wandugu zako wanachunga nyama kule Sekemu. Kwa hiyo ninataka kukutuma kwao.” Yosefu akajibu: “Niko tayari.” 14 Baba yake akamwambia: “Kwenda uwaangalie wandugu zako na nyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamutuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Sekemu, 15 mutu mumoja akamukuta akitangatanga katika mbuga, akamwuliza: “Unatafuta nini?” 16 Yosefu akamujibu: “Ninatafuta wandugu zangu. Tafazali, uniambie pahali wanakochungia nyama.” 17 Yule mutu akamwambia: “Bila shaka wamekwisha ondoka, kwa sababu niliwasikia wakisema kwamba wanakwenda Dotani.” Basi, Yosefu akafuata wandugu zake, akawakuta kule Dotani. 18 Wandugu zake walipomwona akiwa mbali na mbele hajafika karibu, wakafanya mupango wa kumwua. 19 Wakaambiana: “Muangalie! Yule mwota ndoto anakuja. 20 Basi, tumwue na kumutupa ndani ya shimo moja. Kisha tutasema kwamba ameuawa na nyama wa pori. Halafu tutaona hizo ndoto zake zitakuwa namna gani.” 21 Lakini Rubeni aliposikia maneno hayo, akataka kumwokoa toka katika mikono yao. Basi akawaambia wandugu zake: “Tafazali, tusimwue. 22 Musimwange damu. Mumutumbukize katika shimo hili hapa katika mbuga, lakini musimuzuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu kutoka mikono yao na kisha amurudishe kwa baba yake. 23 Yosefu alipowafikia wandugu zake, wao wakamvua kanzu yake. 24 Kisha wakamushika na kumutupa ndani ya shimo. Lakini shimo hilo halikukuwa na maji. 25 Walipoikaa kwa kula wakainua macho na kuona kundi la Waisimaeli wakisafiri kutoka Gileadi kwenda Misri. Ngamia wao walikuwa wakibeba ubani, zeri na manemane. 26 Hapo Yuda akawaambia wandugu zake: “Tutapata faida gani tukimwua ndugu yetu na kuficha damu yake? 27 Afazali tumwuzishe kwa hawa Waisimaeli, lakini tusiguse maisha yake, maana yeye ni ndugu yetu; yeye ni damu moja nasi.” Wandugu zake wakakubaliana naye. 28 Wachuuzi Wamidiani walipofika pahali pale, wale wandugu wakamwondoa Yosefu katika shimo, wakamwuzisha kwa Waisimaeli kwa bei ya vikoroti makumi mbili vya feza; nao wakamupeleka Yosefu Misri. 29 Basi, Rubeni aliporudi kwenye lile shimo, hakumwona Yosefu tena, kwa hiyo akararua nguo zake kwa huzuni, 30 akaendea wandugu zake, akawaambia: “Kijana hayuko, nami niende wapi?” 31 Basi, wakachinja mbuzi, wakaitwaa kanzu ya Yosefu na kuichovya katika damu ya yule mbuzi. 32 Kisha wakamupelekea baba yao ile kanzu, wakamwambia: “Tumeokota kanzu hii. Uangalie kama ni ya mwana wako, au hapana.” 33 Baba yao akatambua hiyo kanzu, akasema: “Ndiyo ni kanzu ya mwana wangu! Bila shaka nyama wa pori amemushambulia na kumukula. Hakika Yosefu ameraruliwa vipandevipande.” 34 Halafu Yakobo akararua nguo zake kwa huzuni, akavaa nguo ya gunia katika kiuno. Akamulilia mwana wake kwa muda wa siku nyingi. 35 Watoto wake wanaume na wanawake wakamufikia kwa kumufariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema: “Uniache. Nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwana wangu, mpaka nitakaposhuka katika kaburi.” Ndivyo baba yake alivyomulilia. 36 Wakati ule, kule Misri, wale Wamidiani wakamwuzisha Yosefu kwa mutu anayeitwa Potifari, mumoja wa wakubwa wa mufalme wa Misri, ambaye alikuwa mukubwa wa waaskari walinzi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo