Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mwanzo 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuzaliwa kwa Isaka

1 Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.

2 Basi, Abrahamu akiwa muzee, Sara akapata mimba, akamuzalia mutoto mwanaume, wakati uleule Mungu aliotaja.

3 Abrahamu akamupa huyo mwana wake ambaye Sara alimuzalia jina la Isaka.

4 Isaka alipotimiza umri wa siku nane, Abrahamu akamutahiri kama alivyoamuriwa na Mungu.

5 Abrahamu alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwana wake Isaka alipozaliwa.

6 Naye Sara akasema: “Mungu amenipatia kicheko; yeyote atakayesikia habari hizi, atacheka pamoja nami.”

7 Kisha akaongeza: “Ni nani angeweza kumwambia Abrahamu kwamba mimi Sara nitanyonyesha watoto? Tena nimemuzalia mutoto mwanaume katika uzee wake!”

8 Isaka akaendelea kukomaa, na siku alipoachishwa kunyonya, Abrahamu akafanya karamu kubwa.


Hagari anafukuzwa

9 Siku moja Sara akamwona Isimaeli, mutoto wa Abrahamu aliyezaliwa na Hagari Mumisri, akicheza na Isaka mwana wake.

10 Basi, Sara akamwambia Abrahamu: “Fukuza mujakazi huyu na mwana wake. Haiwezekani kabisa mutoto wa mujakazi kurizi pamoja na mwana wangu Isaka.”

11 Jambo hili lilimuhuzunisha sana Abrahamu kwa sababu Isimaeli vilevile alikuwa mutoto wake.

12 Lakini Mungu akamwambia Abrahamu: “Usihuzunike kwa sababu ya mutoto huyu, wala huyo mujakazi wako. Jambo lolote Sara atakalokuambia ulifanye. Maana ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.

13 Na juu ya huyo mwana wa mujakazi wako nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa kwa sababu yeye vilevile ni mutoto wako.”

14 Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.

15 Wakati maji yalipomwishia katika lile chupa, Hagari akamulalisha mwana wake chini ya muti.

16 Naye akakwenda kando, akaikaa umbali wa kama metre mia moja hivi, akisema ndani ya moyo wake: “Heri nisimwone mwana wangu akikufa.” Na alipokuwa amekaa pale, mutoto akalia kwa sauti kubwa.

17 Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.

18 Simama umwinue mutoto na kumushika vizuri katika mikono yako, maana nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa.”

19 Mungu akamufumbua Hagari macho, naye akaona kisima cha maji. Akakwenda akajaza chupa maji, akamukunywesha mutoto wake.

20 Mungu akakuwa pamoja na yule mutoto, naye akaendelea kukomaa. Alikaa katika jangwa na akakuwa mupiga upinde hodari sana.

21 Alikuwa akikaa katika jangwa za Parani, na mama yake akamwoea muke kutoka inchi ya Misri.


Agano kati ya Abrahamu na Abimeleki

22 Wakati ule, Abimeleki pamoja na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akamwendea Abrahamu, akamwambia: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.

23 Kwa hiyo uniapie kwa jina la Mungu kwamba hautanidanganya mimi au watoto wangu au wazao wangu. Kadiri mimi nilivyokutendea mema, vivyo hivyo nawe unitendee mema mimi na inchi hii unamokaa.”

24 Abrahamu akasema: “Ninaapa.”

25 Wakati ule Abrahamu alikuwa amemwonya Abimeleki juu ya kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamemunyanganya.

26 Abimeleki akamwambia: “Mimi sijui nani aliyefanya hivyo. Mpaka leo hii wewe haukuniambia, wala mimi sijapata kusikia habari hizi mpaka leo.”

27 Basi, Abrahamu akatwaa kondoo na ngombe akamupa Abimeleki nao wawili wakafanya agano kati yao.

28 Abrahamu akatenga wana-kondoo dike saba.

29 Abimeleki akamwuliza Abrahamu: “Kwa nini unawatenga hao wana-kondoo dike saba?”

30 Abrahamu akamujibu: “Hawa wana-kondoo dike saba ninakupa kwa mukono wangu mwenyewe kama ushuhuda wangu kwamba mimi ndiye niliyechimba kisima hiki.”

31 Kwa hiyo kisima hicho kikaitwa Beri-Seba, maana wote wawili walifanya kiapo pahali pale.

32 Hivyo, wakafanya agano kule Beri-Seba. Abimeleki na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akaondoka na kurudi katika inchi ya Wafilistini.

33 Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beri-Seba, akaomba kwa jina la Yawe, akamwabudu Mungu, Mungu wa milele.

34 Abrahamu alikaa katika inchi ya Wafilistini muda murefu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan