Mwanzo 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyokamilika pamoja na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake. 2 Kwa siku ya saba Mungu alikuwa amemaliza kazi yake yote aliyofanya. Kwa siku ile ya saba Mungu akapumzika kisha kazi yake yote aliyofanya. 3 Mungu akaibariki siku ya saba na kuitakasa, maana kwa siku hiyo Mungu alipumzika kisha kazi yake yote ya kuumba. 4 Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa. Siku ile Yawe Mungu alipoumba mbingu na dunia, Bustani ya Edeni 5 hakukukuwa mimea juu ya inchi wala miti haikukuwa imeota maana Yawe Mungu hakukuwa ameinyeshea inchi mvua, wala hakukukuwa mutu wa kuilima. 6 Maji yalitoka ndani ya udongo yakainywesha inchi yote. 7 Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima. 8 Kisha Yawe Mungu akapanda bustani kule Edeni, upande wa mashariki, na mule akamuweka yule mwanaume aliyemwumba. 9 Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya. 10 Kulikuwa muto kule Edeni uliotiririka maji na kuinywesha ile bustani na kutoka kule muto ule uligawanyika kuwa mito mine. 11 Jina la muto wa kwanza ni Pisoni. Muto ule unazunguka inchi yote ya Havila ambako kuna zahabu. 12 Zahabu ya inchi hiyo ni safi kabisa. Kule vilevile kuna marasi ya bedola na mawe mazuri ya sohamu. 13 Jina la muto wa pili ni Gihoni. Ule unazunguka inchi yote ya Kushi. 14 Jina la muto wa tatu ni Tigre, nao unatiririkia upande wa mashariki wa inchi ya Asuria. Jina la muto wa ine ni Furati. 15 Basi, Yawe Mungu akamutwaa yule mwanaume, akamuweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza. 16 Yawe Mungu akamwamuru yule mwanaume: “Unaweza kula matunda ya muti wowote katika bustani. 17 Lakini usikule matunda ya muti wa kujua mazuri na mabaya, maana siku utakapokula matunda ya muti ule, hakika utakufa.” 18 Kisha Yawe Mungu akasema: “Si vizuri huyu mwanaume kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi wa kumufaa.” 19 Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao. 20 Basi, yule mwanaume akawapa majina nyama wote wa kufugwa, nyama wa pori na ndege wote wa anga. Lakini hakukupatikana musaidizi wa kumufaa. 21 Basi, Yawe Mungu akamuletea yule mwanaume usingizi muzito, na alipokuwa katika usingizi, akatwaa ubavu wake mumoja na kupafunika pahali pale kwa nyama. 22 Na huo ubavu Yawe Mungu alioutoa kwa yule mwanaume akaufanya kuwa mwanamuke, akamuleta kwa huyo mwanaume. 23 Halafu huyo mwanaume akasema: “Kweli! Huyu ni mufupa kutoka mifupa yangu, na nyama kutoka nyama yangu. Huyu ataitwa ‘Mwanamuke’, kwa sababu ametolewa katika mwanaume.” 24 Ndiyo maana mwanaume anamwacha baba yake na mama yake, na kuambatana na muke wake, nao wawili wanakuwa mwili mumoja. 25 Huyo mwanaume na muke wake wote walikuwa uchi, lakini hawakuona haya. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo