Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mwanzo 15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Agano la Mungu na Abramu

1 Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”

2 Lakini Abramu akasema: “Ee Yawe, utanipa nini wakati ninaendelea kuishi bila mutoto, na murizi wangu ni Eliezeri wa Damasiki?

3 Angalia, haujanijalia mutoto. Mutumwa aliyezaliwa ndani ya nyumba yangu ndiye atakayekuwa murizi wangu!”

4 Halafu neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Huyu hatakuwa murizi wako! Mwana wako atakayetoka katika tumbo lako ndiye atakayekuwa murizi wako.”

5 Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”

6 Abramu alimwamini Yawe, naye Yawe akamuhesabu kuwa mwenye haki.

7 Yawe akamwambia Abramu: “Mimi ni Yawe niliyekuleta toka Uri, muji wa Wakaldea, kusudi nikupe inchi hii uirizi.”

8 Lakini Abramu akamwambia: “Ee Yawe, nitajua namna gani kwamba nitarizi inchi hii?”

9 Yawe akamwambia: “Uniletee ngombe dike wa miaka mitatu, mwana-mbuzi dike wa miaka mitatu, kondoo dume wa miaka mitatu, na hua na kitoto cha njiwa.”

10 Abramu akamuletea hao wote, akakata kila nyama vipande viwili, akavipanga katika mistari miwili, vikielekeana. Lakini ndege hakuwakata vipande viwili.

11 Na tai waliposhuka juu ya mizoga hiyo, Abramu akakuwa anawafukuza.

12 Jua lilipokuwa likitua, Abramu akashikwa na usingizi muzito. Hofu na giza nene vikamufunika.

13 Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.

14 Hata hivyo, nitaazibu taifa watakalotumikia na kwa mwisho watatoka wakiwa na mali nyingi.

15 Lakini wewe mwenyewe utaishi maisha marefu na kufa kwa amani.

16 Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”

17 Jua lilipokwisha kutua na giza kuingia, furu inayofuka moshi na mwenge unaowaka moto vikapita katikati ya vile vipande vya nyama.

18 Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,

19 ni kusema inchi za Wakeni, Wakenizi, Wakadimoni,

20 Wahiti, Waperizi, Warefaimu,

21 Waamori, Wakanana, Wagirgasi na Wayebusi.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan