Mwanzo 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Abramu anamwokoa Loti 1 Kwa wakati ule, mufalme Amurafeli wa Sinari, mufalme Arioki wa Elasari, mufalme Kedorilaomeri wa Elamu na mufalme Tidali wa Goimu, 2 wakapigana vita na Bera mufalme wa Sodoma, na Birsa mufalme wa Gomora, Sinabu mufalme wa Adima, Semeberi mufalme wa Seboimu, na mufalme wa Bela ni kusema Soari. 3 Wafalme wale watano waliyaunganisha majeshi yao katika bonde la Sidimu, ni kusema bahari ya Chumvi. 4 Kwa muda wa miaka kumi na miwili walikuwa wakimutii mufalme Kedorilaomeri, lakini katika mwaka wa kumi na tatu, wakamwasi. 5 Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu, 6 na Wahori kule kwenye mulima wa Seiri, wakawafukuza mpaka Eliparani, kwa mupaka wa jangwa. 7 Kisha wakarudi nyuma mpaka Enimisipati ni kusema Kadesi, wakapiga inchi yote ya Waamaleki, na kuwashinda Waamori waliokaa Hasasoni-Tamari. 8 Halafu mufalme wa Sodoma, mufalme wa Gomora, mufalme wa Adima, mufalme wa Seboimu na mufalme wa Bela 9 ni kusema Soari, wakaingia katika vita katika bonde la Sidimu kupigana na Kedorilaomeri mufalme wa Elamu, Tidali mufalme wa Goimu, Amurafeli mufalme wa Sinari na Arioki mufalme wa Elasari: wafalme wane kupigana na wafalme watano. 10 Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima. 11 Basi, wale walioshinda, wakanyanganya mali yote ya Sodoma na Gomora, hata na mazao yao, wakajiendea. 12 Wakamukamata hata Loti mwana wa ndugu ya Abramu aliyekuwa anakaa Sodoma, pamoja na mali yake, wakajiendea. 13 Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu. 14 Abramu alipopata habari kwamba mwipwa wake amekamatwa kuwa mufungwa, akatoka na watu wake mashujaa mia tatu na kumi na wanane waliozaliwa katika nyumba yake, akawafuatilia waadui mpaka Dani. 15 Kule, akagawanya jeshi lake katika makundi. Usiku, akawashambulia waadui zake, akawashinda na kuwafukuza mpaka Hoba, upande wa kaskazini wa Damasiki. 16 Basi, Abramu akakomboa mali yote iliyonyanganywa na waadui, na kumukomboa mwipwa wake Loti, mali yake, pamoja na wanawake na watu wengine. Melkisedeki anamubariki Abramu 17 Abramu aliporudi kisha kumushinda mufalme Kedorilaomeri na wenzake, mufalme wa Sodoma akatoka na kwenda kukutana naye katika bonde la Sawe ni kusema bonde la Mufalme. 18 Naye Melkisedeki, mufalme wa muji wa Salemu, ambaye alikuwa kuhani wa Mungu Mukubwa, akaleta mukate na divai, 19 akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia! 20 Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. 21 Mufalme wa Sodoma akamwambia Abramu: “Unipe wale watu, lakini ujitwalie mali yote wewe mwenyewe.” 22 Lakini Abramu akamwambia mufalme wa Sodoma: “Ninaapa kwa Yawe, Mungu Mukubwa, aliyeumba mbingu na dunia, 23 kwamba sitatwaa uzi au kamba ya kiatu, wala chochote kinachokuwa chako, kusudi usijivune na kusema kwamba umenitajirisha. 24 Basi, sitatwaa kitu chochote isipokuwa tu vile vitu ambayo vijana wangu walikula na sehemu ya wale waliokuwa pamoja nami – Aneri, Eskoli na Mamure – ambao wana haki nayo.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo