Mwanzo 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu anamwita Abramu aache inchi yake 1 Basi, Yawe akamwambia Abramu: “Ondoka katika inchi yako, acha jamaa yako na nyumba ya baba yako, uende katika inchi nitakayokuonyesha. 2 Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka. 3 Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.” 4 Kwa hiyo, Abramu akaondoka kama vile Yawe alivyomwamuru, na Loti akakwenda pamoja naye. Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi saba na mitano alipotoka Harani. 5 Alitwaa Sarai muke wake, na Loti mwana wa ndugu yake, pamoja na mali yao yote na watu wote waliokuwa wamejipatia kule Harani, wakaondoka kuelekea inchi ya Kanana. Walipoingia katika inchi ya Kanana, 6 Abramu akapita katikati ya inchi mpaka Sekemu, pahali patakatifu, penye muti wa mwelo wa More. Wakati ule, Wakanana walikuwa ndio wenyeji wa inchi hiyo. 7 Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea. 8 Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake. 9 Kisha Abramu akaendelea kusafiri kuelekea upande wa Negebu. Abramu katika inchi ya Misri 10 Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda. 11 Alipokaribia Misri, Abramu akamwambia Sarai muke wake: “Ninajua kwamba wewe ni mwanamuke muzuri na wa kuvutia. 12 Wamisri watakapokuona watasema: ‘Huyu ni muke wake’, kisha wataniua lakini wewe watakuacha muzima. 13 Basi, uwaambie kwamba wewe ni dada yangu kusudi mambo yaniendee vema, niachwe niishi kwa ajili yako.” 14 Basi, Abramu alipofika Misri, wenyeji wa kule wakaona kwamba Sarai ni mwanamuke muzuri sana. 15 Wakubwa wa mufalme wa Misri walipomwona Sarai, wakamusifia kwa mufalme. Basi, Sarai akapelekwa ndani ya nyumba ya yule mufalme. 16 Naye akamutendea Abramu mema kwa ajili ya Sarai. Akamupa kondoo, ngombe, punda dume, watumishi na wajakazi, punda dike na ngamia. 17 Lakini Yawe akamutesa na watu wote wa nyumba yake kwa mapigo makali kwa sababu ya Sarai, muke wa Abramu. 18 Mufalme akamwita Abramu, akamwuliza: “Ni kitu gani hiki ulichonitendea? Mbona haukunijulisha kwamba Sarai ni muke wako? 19 Kwa nini ulisema ni dada yako hata nikamutwaa kuwa muke wangu? Basi, sasa muke wako ule. Umutwae, ujiendee!” 20 Kisha mufalme yule akawaamuru watu wake wasindikize Abramu katika njia akikuwa na muke wake na mali yake yote. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo