Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Muhubiri 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mainzi waliokufa wanaharibu na kunukisha marasi; upumbafu kidogo unapoteza hekima na heshima.

2 Moyo wa mwenye hekima unamwongoza kutenda mambo yanayokuwa sawa; lakini mutu mupumbafu anapotoshwa na moyo wake.

3 Hata anapopita katika njia, anakosa akili, anamwambia kila mutu kwamba yeye ni mupumbafu.

4 Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.

5 Kuna uovu niliotambua hapa chini ya jua, uovu unaosababishwa na watawala:

6 wapumbafu wanapewa kazi za madaraka ya juu, na watajiri wanakamata nafasi za mwisho.

7 Nimeona watumwa wanapanda juu ya farasi, na wakubwa wanatembea kwa miguu kama watumwa.

8 Yeye anayechimba shimo anatumbukia ndani yake mwenyewe, anayebomoa ukuta anaumwa na nyoka.

9 Muchonga mawe anaumizwa nayo, mukata kuni anapatwa na hatari.

10 Nguvu nyingi zaidi zinahitajika kwa mutumiaji wa shoka lisilonolewa, lakini kutumia hekima kunamufanya mutu afanikiwe.

11 Nyoka ya muchawi ikiuma mbele haijachochewa, hakuna faida tena kwa muchawi.

12 Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.

13 Mupumbafu anaanza kusema kwa maneno ya kijinga, na kumaliza masemi yake kwa wazimu wa hatari.

14 Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.

15 Mupumbafu anachokeshwa kwa kutoa jasho, hata hajui njia ya kwenda katika muji.

16 Ole wako, ewe inchi, mutawala wako akiwa kijana, na viongozi wako wakifanya karamu asubui.

17 Heri yako, ewe inchi, mutawala wako akiwa mutu wa heshima, na viongozi wako wakifanya karamu wakati unaofaa, kwa kujipatia nguvu na si kujilewesha.

18 Kutokana na uvivu wa mutu, paa ya nyumba inaanguka; kwa sababu ya uregevu, nyumba inavuja.

19 Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.

20 Usimutukane mutawala hata ndani ya moyo wako, wala usimutukane tajiri hata ndani ya chumba chako cha kulala, maana ndege atapeleka sauti yako, kiumbe kinachoruka kitatangaza maneno yako.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan