Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Muhubiri 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maisha ni bure

1 Maneno haya ni ya Muhubiri mwana wa Daudi, aliyekuwa mufalme kule Yerusalema.

2 Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure!

3 Mwanadamu anafaidia nini kwa jasho lake lote hapa chini ya jua?

4 Kizazi kimoja kinapita na kingine kinakuja, lakini dunia inadumu milele.

5 Jua linachomoza na kutua; linarudi haraka kwa pahali linapotokea.

6 Upepo unavuma tokea kusini, unazunguka mpaka kaskazini. Unazungukazunguka katika mwendo wake, kisha unarudia tena katika muzunguko wake siku zote.

7 Mito yote inatiririkia ndani ya bahari, lakini bahari haijai hata kidogo; kule ambako mito inatiririkia ndiko kule inaendelea kwenda.

8 Mambo yote yanasababisha muchoko, muchoko mukubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.

9 Yaliyokuwa ndiyo yatakayokuwa, yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka. Chini ya jua hakuna jambo jipya.

10 Watu wanasema: “Angalia jambo hili ni jipya”, kumbe limekwisha kutendeka zamani za kale.

11 Hakuna mutu anayekumbuka mambo ya zamani, wala atakayekumbuka yatakayotukia kisha.


Ujuzi wa Muhubiri

12 Mimi Muhubiri, nilikuwa mufalme wa Israeli, kule Yerusalema.

13 Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.

14 Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!

15 Kitu kilichokunjama hakiwezi kunyooshwa. Kitu kisichokuwa hakiwezi kuhesabiwa.

16 Basi, nikafikiri nikisema: “Nimejipatia hekima nyingi zaidi kupita wote waliopata kutawala Yerusalema mbele yangu. Kweli, ninajua hekima na maarifa ni nini.”

17 Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.

18 Maana katika kuwa na hekima nyingi kuna wasiwasi; na anayeongeza maarifa zaidi anaongeza huzuni zaidi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan