Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mika 6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Malalamiko ya nabii

1 Musikilize jinsi Yawe anavyosema: Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima, navyo vilima visikie sauti yako.

2 Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.

3 Anasema hivi: Enyi watu wangu, nimewatendea nini? Nimewachokesha kwa kitu gani? Munijibu!

4 Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.

5 Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!

6 Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?

7 Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?


Jibu la nabii

8 Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.

9 Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.

10 Nitavumilia maovu yaliyolundikwa ndani ya nyumba yao, mali zilizopatikana kwa udanganyifu, na matumizi ya vipimo vya udanganyifu, jambo ambalo ni chukizo?

11 Ninaweza kusema kwamba hawana kosa watu wanaotumia vipimo vya udanganyifu na mawe ya kupimia yasiyokuwa ya kweli?

12 Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.

13 Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini, na kuwaangamiza kwa sababu ya zambi zenu.

14 Mutakula lakini hamutashiba; njaa itazidi kuwa katika tumbo yenu. Mukiweka akiba haitachungwa, na mukichunga kitu nitakiharibu kwa vita.

15 Mutapanda mbegu, lakini hamutavuna. Mutakamua mafuta ya zeituni, lakini hamutatumia mafuta hayo. Mutakamua zabibu, lakini hamutakunywa divai hiyo.

16 Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan