Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mika 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mutawala mupya kutoka Betelehemu

1 Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.

2 Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.

3 Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.

4 Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Ukombozi na azabu

5 Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.

6 Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima wataenea kati ya mataifa mengi, watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe, kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani ambayo hayasababishwi na mutu wala kumutegemea mwanadamu.

7 Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.

8 Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.

9 Wakati ule, nitawaondoa farasi wenu, na kuyaharibu magari yenu ya vita. –Ni ujumbe wa Yawe.–

10 Nitaiharibu miji ya inchi yenu, na kubomoa vikingio vyenu.

11 Nitakomesha matendo yenu ya uchawi, nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.

12 Nitaziharibu sanamu zenu, na nguzo zenu za ibada; nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.

13 Nitaziongoa sanamu za Ashera kutoka kwenu, na kuiangamiza miji yenu.

14 Kwa hasira na kasirani yangu, nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan