Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hekima na upumbafu

1 Hekima amejenga nyumba yake, nyumba yenye nguzo saba.

2 Amechinja nyama wa karamu, divai yake ameitayarisha, ametandika meza yake.

3 Amewatuma wajakazi wake katika muji waite watu kutoka kwenye vilele vya milima:

4 “Yeyote anayekuwa mujinga akuje hapa!” Na yeyote anayekuwa mupumbafu unamwambia:

5 “Kuja ukule chakula, na ukunywe divai niliyotengeneza.

6 Achana na ujinga upate kuishi; fuata njia ya akili.”

7 Anayemwonya mwenye kiburi anapata mazarau, anayekaripia mwovu anajiletea matusi.

8 Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.

9 Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.

10 Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima; na kumujua yule Mutakatifu ni kupata akili.

11 Kwa musaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa; utaongezewa miaka mingi katika maisha yako.

12 Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe; kama ukiizarau, wewe mwenyewe utapata hasara.

13 Mwanamuke mupumbafu ana kelele, hajui kitu wala hana haya.

14 Anaikaa kitako kwenye mulango wa nyumba yake, anaweka kiti chake pahali pa juu katika muji,

15 na kuwaita watu wanaopita katika njia, watu wanaokwenda kwenye shuguli zao:

16 “Yeyote anayekuwa mujinga akuje hapa!” Na yeyote anayekuwa mupumbafu anamwambia:

17 “Maji yaliyoibwa ni matamu sana; mukate unaokuliwa kwa siri ni muzuri sana.”

18 Lakini mujinga hajui kwamba mule muna wafu, wageni wa mwanamuke yule wako chini katika kuzimu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan