Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mashauri ya mufalme

1 Maneno ya mufalme Lemueli. Mashauri aliyopewa na mama yake:

2 Nikuambie nini mwana wangu? Nikuambie nini mwana wangu niliyezaa? Nikuambie nini wewe niliyeomba kwa Mungu?

3 Usimalize nguvu zako kwa wanawake, usiwape mali yako wale wanaoangamiza wafalme.

4 Haifai, ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai, wala wakubwa kutamani vileo.

5 Wakikunywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.

6 Umupe mutu anayekaribia kufa kinywaji kikali, uwape divai wale wenye huzuni tele;

7 wakunywe na kusahau umasikini wao, wasikumbuke tena taabu yao.

8 Lakini wewe, useme kwa ajili ya wote wanaokuwa bubu; na kutetea haki za wote wasiojiweza.

9 Sema kwa ajili yao na kuamua kwa haki, linda haki za wamasikini na wakosefu.


Muke mwema

10 Muke mwema atapatikana wapi? Bei yake ni kali kuliko ushanga!

11 Mume wake anamwamini kwa moyo na hatakosa faida.

12 Hamutendei mume wake mabaya hata kidogo, lakini anamutendea mazuri maisha yake yote.

13 Anatafuta sufu na kitani, na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.

14 Yeye ni kama mashua za biashara: analeta chakula chake kutoka mbali.

15 Anaamuka mbele ya mapambazuko kwa kutayarishia jamaa yake chakula na kuwagawanyia kazi watumishi wake.

16 Anafikiri kununua shamba, kisha analinunua, na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.

17 Yuko tayari kufanya kazi kwa nguvu na kuimarisha mikono yake.

18 Anatambua kwamba shuguli zake zina faida; anafanya kazi hata usiku kwa mwangaza wa taa yake.

19 Anasokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe, kwa vidole vyake mwenyewe anasuka nguo zake.

20 Anafungua mukono wake kwa kuwapa wamasikini, ananyoosha mukono kwa kusaidia wakosefu.

21 Haogopi juu ya jamaa lake wakati wa baridi kali, maana kila mutu yuko na nguo za kutosha.

22 Anajitengenezea matandiko, nguo zake ni za rangi nyeusi-nyekundu za kitani safi.

23 Mume wake ni mutu mwenye kuheshimiwa katika baraza, anapoikaa katikati ya wazee wa inchi.

24 Mwanamuke huyu anatengeneza nguo na kuziuzisha, anawauzishia wachuuzi mikaba.

25 Nguvu na heshima ndizo sifa zake. Anacheka anapofikiri juu ya wakati unaokuja.

26 Anafungua kinywa kwa kusema kwa hekima; anawashauri wengine kwa wema.

27 Anachunguza yote yanayofanyika katika nyumba yake; hakai bure hata kidogo.

28 Watoto wake wanaamuka na kumushukuru, mume wake anaimba sifa zake.

29 Anasema: “Wanawake wengi wametenda mambo ya ajabu, lakini wewe umewashinda wote.”

30 Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii, lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.

31 Jasho lake linastahili kulipwa. Shuguli zake zinapaswa kuheshimiwa popote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan