Mezali 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maonyo kwa vijana 1 Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu. 2 Maana vitakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi. 3 Wema na uaminifu zisitengane nawe. Uvifunge katika shingo lako; uviandike ndani ya moyo wako. 4 Hivyo utakubaliwa na kusifiwa, mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu. 5 Umutumainie Yawe kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe. 6 Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako. 7 Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu. 8 Hiyo itakuwa dawa kwa mwili wako, na kitu cha kutuliza mifupa yako. 9 Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote. 10 Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano, na mitungi yako itafurika na divai mupya. 11 Mwana wangu, usizarau azabu ya Yawe, wala usiuzike kwa maonyo yake; 12 maana Yawe anaonya yule anayemupenda, kama vile baba anavyomwonya mwana wake mupenzi. 13 Heri mutu anayetambua hekima, mutu yule anayepata ufahamu. 14 Hekima ni bora kuliko feza, ina faida kuliko zahabu. 15 Hekima ni ya maana sana kuliko mawe ya bei kali, hakuna kitu unachotamani kinachoweza kulingana nayo. 16 Itakupa maisha marefu, mali na heshima. 17 Njia zake ni za kupendeza, zote zinaelekea kwenye amani. 18 Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo. 19 Kwa hekima Yawe aliweka misingi ya dunia, kwa akili aliziimarisha mbingu. 20 Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka, na mawingu yakadondosha umande. 21 Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako, 22 navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako, na pambo zuri katika shingo lako. 23 Halafu utaweza kwenda zako kwa usalama, wala muguu wako hautajikwaa. 24 Unapolala, hautakuwa na hofu, utapata usingizi muzuri. 25 Usiogope juu ya tisho la rafla, wala shambulio kutoka kwa waovu, 26 maana Yawe ndiye atakayekutegemeza, atakuepusha usipate kunaswa katika mutego. 27 Usimunyime mutu anayehitaji musaada, ikiwa una uwezo wa kufanya hivyo. 28 Usimwambie jirani yako “Kwenda na urudie kesho, halafu nitakupatia” wakati wewe unaweza kumupa anachohitaji leo. 29 Usipange maovu juu ya jirani yako anayeishi karibu nawe bila wasiwasi. 30 Usigombane na mutu bila sababu, ikiwa hajakuzuru kwa lolote. 31 Usimwonee wivu mutesaji, wala usiige mwenendo wake. 32 Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake. 33 Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki. 34 Yeye anazarau wenye mazarau, lakini anakubali wanyenyekevu. 35 Wenye hekima watavuna heshima, lakini wapumbafu watapata haya. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo